GuidePedia

0


Mkazi   mmoja  wa  kijiji  cha mwela wilayani rungwe  mkoani  mbeya   Sela   mwakasendele  mbogoso   miaka  {33} ameingia  kwenye  wakati mgumu  baada  ya kunyofolea    kwa  kung’atwa  sikio na   jicho  lake  la kushoto  na mumewe   fati mwasumbwe   kutokana na kile  kilicho daiwa  kuwa  ni wivu wa  kimapenzi.

 Hayo  yamejili   usiku wa  kuamkia   janual {1}   mwaka huu  ambapo   bila kujua  hili wala lile  mama   huyo alijikuta  akiingia  kwenye wakati  mgumu baada  ya  kurejea nyumbani kwake  majira  ya  usiku  wa manane   huku  akiwa  amelewa  pombe  kufuatia kileo hicho kimepelekea kutofautiana na mumewe hivyo  kuanza  kushambuliwa na mume ikiwa  ni pamoja  na   kunyofolewa kwa  kung’atwa  sikio  na jicho la  kushoto  na kupelekea  kupoteza   damu nyingi zaidi.

Mashuhuda wa  waliokuwepo eneo la tukio wamesema tukio hilo limetokea  baada  ya mama  huyo  kuchelewa  kurejea  nyumbani   kwake  ndipo kutokana  na hali hiyo mume  alijikuta  amejawa na hasira   na   kuanza  kumuadhibu  vikali  mkewe.

Aidha alisema   watu  hao kugombana  imekuwa  kawaida  yao   na kwamba  kila ifikapo  nyakati  ya  usiku  huwa  wanawasumbua  kwa   kuwapigisha  kelele   na  kuamua kufikia  hatua  ya  kuwakamata   kwa  kuwa fikisha  kwenye   kwenye vyombo vya sheria ili kutatua tatizo lao.

Kwa  upande wa  mama   huyo  alisema     chanzo  ni baada  ya  mumewe    kumuhisi  kwamba  mkewe  ana wanaume  wengine   na  kwamba  yeye  huwa  anachelewa  virabuni kuuza   pombe .

Kwa  upande wake  mume  na     mwanamke   huyo amesema  amefikia  hatua hiyo  baada ya kuchoka  na  tabia za mkewe  kwani kila  siku amekuwa mtu wa  kurumbana naye   na kwamba   ili kupunguza    kiburi chake akamua  kumuweka alama  ya   kutosha  ili iwe fundisho  na kwa  wengine.

Mtendaji wa  kijiji  hicho   Neema  Ipopo licha ya  kukiri  kutokea  kwa  tukio hilo amesema mpaka sasa  Serikali imewapatia     kibari  cha  kwenda   hospital  kwaajili ya kutibiwa  huku  hatua  zingine  za  kisheria   zikichukuliwa  dhidi yao.

                  Na, Baraka Lusajo rungwe


Post a Comment

 
Top