GuidePedia

0


Afisa wa kilimo wilaya ya Mbinga Bw, Yonasi Nyoni alipokuwa akiongea na mwandishi wa Mtandao huu Ofisini kwake.

Baadhi ya wakulima waliyoathirika na pembejeo hizo ambao wengine ni viongozi wa serikali ya mtaa katika wilaya hiyo walipokuwa wakiongea na mwandishi wa Mtansdao huu.

Afisa ukaguzi wa pembejeo kutoka katika ofisi ya kilimo wilaya ya Mbinga Bw, Andrew Chiwinga.

 



BAADHI ya wakulima wilayani Mbinga mkoani Ruvuma wameiomba serikali kutowaonea aibu wafanyabiashara  wa Pembejeo wenye tamaa ya kujipatia faida kubwa kwa kuuza bidhaa feki, hivyo kuhatarisha usalama wa chakula na kuwapunguzia mavuno.

Hayo yalisemwa jana na wakulima hao walipohojiwa na Mtandao huu wamesema,serikali inapaswa kusimamia usambazaji wa pembejeo kote nchini ili kudhibiti uingizwaji wa bidhaa feki ambao umeanza kushamiri katika kipindi cha hivi karibuni.

John Kapinga mkulima katika kitongoji cha Lusaka alisema  kitendo cha kuuziwa pembejeo feki wakulima, kinawarudisha nyuma na kuwafanya washindwe kutimiza malengo yao ya kiuchumi ikiwa ni pamoja na kukabiliana na  harakati za kuondoa umasikini.

 “katika msimu uliopita nilinunua mbolea aina ya chumvi chumvi (SA), lakini nilipoiweka shambani haikuonesha matokeo mazuri, hali ambayo ilinifanya nisipate mavuno mazuri  ikilinganisha nay a misimu mingine” alisema Kapinga.

Kapinga alisema serikali isiwaachie wafanyabiashara wafanye watakavyo na kwamba wakiachiwa  wanaweza kuliangamiza taifa kwa kulikosesha chakula na kudidimiza uchumi wa wakulima.

Akizungumzia suala hilo Ofisa Kilimo wilayani Mbinga Yonasi Nyoni alisema tatizo hilo limejitokeza katika kijiji cha Liula ambapo ofisi yake ilichukua hatua ya kwenda kukagua ambapo hali ya mazao shambani walikuta ni mbaya ukilinganisha na matarajio baada ya kuweka mbolea hiyo na ndipo walipochukua sampuli ili kuzifanyia utafiti.

Amesema mbolea hiyo aina ya Chumvichumvi ilipopimwa ilikutwa ina kiwango kidogo cha Nitrojen cha asilimia mbili badala ya 21, kiwango ambacho hakiwezi kuleta tija shambani, hali hiyo ilifanya muuzaji kuchukuliwa hatua kwa kufunguliwa mashitaka katika mahakama ya mwanzo Mbinga na kesi No. 43/2014.

Amewataja washitakiwa katika kesi hiyo kuwa ni Hamisi Nakanga na Dastan Kombe ambao walikuwa wakiwakopesha wakulima mbolea hizo kwa makubaliano ya wakulima kulipa mahindi gunia mbili na robo za mahindi baada ya mavuno ya msimu unaokuja.

 Nyoni alisema serikali wilayani hapa imeweka mkakati wa kukagua pembejeo katika maduka kila baada ya miezi mitatu ikiwa ni pamoja na kuwasajili mawakala wauzaji pembejeo na kuwahamasisha wakulima kununua pembejeo kwa mawaka waliosajiliwa na wadai stakabadhi kila wanunuapo bidhaa hizo.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Mbinga Oska Yapesa alikiri kupokea malalamiko ya wananchi kuhusiana na kuuziwa mbolea feki na kwamba hata yeye aliwahi kuuziwa  Mbegu feki huko Dar es salaam,  ambazo alipopanda hazikuota akalazimika kupanda upya.
                          


                                  Na Lumemo blog

 

 



Post a Comment

 
Top