GuidePedia

0


Serikali kupitia idara ya afya   katika Halmashauri ya  Busokelo wilayani  Rungwe  mkoani Mbeya  imetoa   kiasi ya cha  sh. 4000000/=    kwa  ajili ya  ujezi wa zahanati ya Matamba ambayo  inaendelea  kujengwa  kwa nguvu za wananchi.

Akizungumza  na mwandishi wetu  mganga  mkuu wa   Harimashauri ya wilaya  ya Busokelo wilayani humo  Gibert Tarimo alisema     kutokana  na  wananchi    wa  kijiji  hicho kuonyesha moyo katika  ujenzi  wa   zahanati  yao  baada ya kusumbuka kwa muda mrefu  katika   kutafuta  huduma    ya matibabu,  serikali   kupitia bidala hiyo  imetoa   shiringi  milioni  nne  kwa  ajili   ya kusadia  kumalizia   ujenzi  wa   zahanati hiyo.
 “  Serikali  kupitia idara  ya afya iliona  ni vyema  ikashirikiana  na  wananchi wa kijiji hiki katika ujenzi wa kituo chao cha  afya  kwakuwapatia msaada  wa pesa  kiasi  cha  shilingi milioni nne ambazo  zitatumika  kumalizia  ujenzi wa zahanati hii
Adha   Tarimo aliwataka wanachi kuendelea na moyo   huo   na kusema kufanikisha  kwa  kazi  hiyo  kuta tegemea na  uelekezi wa nguvu zao  katika  ujenzi wa  zahanati hiyo.

Jampyoni  mbuguru   ambaye ni  mwanachi  wa kijiji hicho mbali na kuupongeza  uongozi   huo kwa jitihada walizo zionesha alisema uwepo wa kituo hicho   utasaidia wao   kupunguza  vifo  vya  watoto  na ndugu zao ambao walikuwa  wakipatwa na  maafa wakati  wa kuwakimbiza katika vituo vya  afya .

“ sisi  kama  wananchi  tuliamua kuanza  ujenzi wa kituo hiki  baada ya  kutembea  umbali mrefu katika kutafuta  huduma  muhimu  ya   afya ambayo inapatika  zaidi  ya kilometa  {7}  na  kusema  wakati mwingine  ndugu zetu wamekuwa wakifia njiani  pindi  tunapowapeleka katika  vituo  hivyo kwa matibabu zaidi na  ukizingatia  kuwa  katika  maeneo  haya  hakuna usafiri zaidi ya baisikeli”. alisema Mbunguru.

Mwenyekiti wa  kijiji  hicho     Johan mwakyoma  kwa  upande wake alisema   katika kukamilisha  hatua  hiyo  walijipangia   kutoa  kiasi cha shiringi  elfu thelatini kwa  kila mmoja  30000/= ambazo  wanazitoa   kwa awamu  sita na kusema  mpaka sasa  wamemaliza hatua  ya  linta  na  wamenza   ufyatuaji wa tofari na kuwalipa mafundi.

                               Na, Baraka lusajo Rungwe

Post a Comment

 
Top