Umoja wa Madereva wa Mabasi Tanzania[UWAMATA]kanda ya Mbeya
wamelalamikia Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani na Mamlaka ya
Usafirishaji[SUMATRA] Mkoa wa Mbeya kwa kuwanyanyasa wawapo kazini.
Tamko
hilo limetolewa na Mwenyekiti wa Madereva kanda Damas Mwandumbya katika ukumbi
wa Miami iliopo Kata ya Ilomba Jijini Mbeya mbele ya Mgeni rasmi Mkuu wa Polisi
Mkoa ambaye aliwakilishwa na Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Mbeya Robert Mayala.
Waliotuhumiwa
kula rushwa ni pamoja na Askari Polisi wa kikosi cha Usalama Barabarani wa
Wilaya za Rungwe na Mbeya ambapo majina yao yalitajwa mbele ya kikao hicho pamoja
na Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Mbeya Butusyo Mwambelo ambaye imedaiwa
kuwapa malengo Askari wake ili mgao afikishiwe kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Mbeya.
Mgao
mwingine wa pesa hizo umetajwa kwenda kwa Mkuu wa Usalama Barabarani nchini na
kila Dereva anapokamatwa au kusimamishwa hulazimika kutoa shilingi elfu tano au
zaidi katika kila kituo anachosimamishwa ndipo gari huendelea na safari.
Hali
hiyo husababisha Madereva kujaza abiria ili kukidhi malengo ya waajiri na
kumudu kulipa Askari wa Usalama Barabarani na kama wasipotoa hukamatwa na
kutozwa faini au kupelekwa mahabusu hali inayowafanya kufanya kazi katika
mazingira magumu.
Aidha
Madereva hao walimtuhumu Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa Mbeya kwa kuwafukuza
ofini kwake pindi wanapohitaji huduma na
kuwa na lugha chafu inayowadhalilisha madereva hivyo mara kadhaa kugoma au
kutishia kugoma kutokana na kauli za kiongozi huyo.
Mbali
ya shutuma hizo kwa Jeshi la Polisi SUMATRA walilalamikiwa kwa kuruhusu magari
ya aina ya NOAH ambayo yameanza kusafirisha abiria bila kukidhi vigezo hali
inayosababisha baadhi ya magari ya abiria aina ya HIACE kushindwa kufanya kazi
kutokana na magari hayo kufanya kazi kiholela huku Jeshi la Polisi na SUMATRA
wakifumbia macho.
Akijibu
tuhuma hizo Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Mbeya Robert Mayala aliwapa fursa
wanaotuhumiwa kujieleza mbele ya mkutano huo uliojumuisha madereva wa COASTER
na HIACE ambapo Mkuu wa Usalama Barabarani alikanusha kuwafukuza madereva
ofisini kwake bali alidai kuwa viongozi wanatetea wahalifu hali hiyo
isipodhibitiwa itasababisha ajali ambazo zinaweza kuepukika.
Hata
hivyo Butusyo aliomba radhi endapo amewafukuza ofisini kwake madereva hiyo
imekuja kutokana na dharau za baadhi ya maderva ambao wamekuwa wakidharau
Askari wake hata yeye amedharauliwa kwa madereva kujaza abiria licha ya kupewa
onyo.
Kwa
upande wake Meneja wa SUMATRA amesema kuwa amepokea malalamiko yao na kuahidi
kuyafanyia kazi malalamiko yao lakini pia Madereva wafuate sheria ili kuondoa
mvutano usio wa lazima kwani madereva ni sehemu ya jamii ambao wana mchango
mkubwa kwa Taifa.
Mkuu
wa upelelezi Mkoa wa Mbeya Robert Mayala amekiri kupokea malalamiko yao na
kwamba Jeshi la Polisi litakutana na Askari wanaolalamikiwa hasa wa Wilaya ya
Rungwe na amemwagiza Mkuu wa usalama Barabarani kurekebishwa kasoro zote ili
kila upande ufanye kazi kwa amani.
Alihitimisha
kwa kuwataka Madereva kutii sheria bila shuruti ili kuepusha ajali na kuwataka
madereva wakatae kutoa rushwa na Askari atakaye walazimisha watoe taarifa kwake
ambapo aliwapatia namba zake za simu yake ili kupata taarifa kwa haraka.
Post a Comment
Post a Comment