GuidePedia

0
MWALIMU wa shule ya msingi Katani wilayani Nkasi mkoani Rukwa Ringtone Rayson (36)amehukumiwa kwenda kutumikia kifungo  cha miaka miwili jela au kulipa faini ya Tshs,100,000 kwa kosa la kufumaniwa na mke wa mtu Beata sangu (31) na kumjeruhi mme wa mwanamke huyo kwa mapanga na msumeno iliyokuwemo ndani ya nyumba hiyo

Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya Nkasi Ramadhani Rugemalila mwendesha mashitaka wa jeshi la polisi 

Hamimu Gwelo alisema kuwa mtuhumiwa mnamo oktoba 12 mwaka jana  majira ya saa 3 usiku mme wa mwanamke huyo  alipata taarifa kutoka kwa msiri wake kuwa mwalimu huyo aliingia ndani ya nyumba yake na kufanya mapenzi na mkewe wakati yeye alipokuwa amekwenda kulala kwa mke mdogo

Alisema kuwa mme wa mwanamke huyo Richard Feruzi (33) baada ya kupata taarifa hizo alikwenda kumtafuta mdogo wake  Stanslaus Feruzi na viongozi wa mtaa ule kwa lengo la kwenda kumfumania mwalimu huyo na baada ya wote kufika katika nyumba ile walipiga hodi lakini hawakufungua na ndipo walipoanza kuvunja mlango ili waweze kumkamata mtuhumiwa aliyekuwa katika nyumba hiyo

Mwendesha mashitaka huyo wa jeshi la polisi aliifafanulia mahakama hiyo kuwa wakati mlango ule ulipokuwa ukivunjwa mtuhumiwa ambaye ni mwalimu aliamua kuchukua panga na msumeno vilivyokuwamo katika nyumba hiyo na kuamua kutoka na kuanza kuwashambulia kwa mapanga mme wa mwanamke huyo Richard Feruzi na mdogo wake Stanslaus Feruzi na kuwapatia majeraha makali na kukimbizwa hospitalini kwa matibabu

Baada ya mtuhumiwa kukiri kutenda kosa hilo mahakama hiyo ilimuadhibu mtuhumiwa kwenda jela miaka miwili au kulipa faini ya Tshs,100,000 na fidia ya Tshs,150,000 kwa kila majeruhi kati ya wale wawili mme na mdogo wa mme kutokana na majeraha waliyoyapata

Hakimu wa mahakama hiyo Bw,Rugemalila alisema kuwa mtuhumiwa alitiwa hatiani chini ya kifungu  No,225 sura ya 16 ya kanuni ya adhabu

Mtuhumiwa baada ya kutiwa hatiani na mahakama hiyo alilipa faini ya Tshs,100,000 na fidia zote na jumla ya Tshs,400,000 zilitolewa katika mahakama hiyo na kuachiwa huru

                             Na, Lumemo blog


                                        

Post a Comment

 
Top