GuidePedia

0

Mkaguzi mkuu wa Osha Tanzania bara Dr, Akwilina Kayumba na Meneja wa Osha kanda ya nyanda za juu kusi Eng, George Chali wakiwa studio za Radio Bomba fm na mtangazaji na mwandishi wa habari wa bomba fm Martha Haule katika kipindi cha Amka Bomba kinachoruka asubuhi kuanzia saa kumi na mbili na nusu mpaka saa nne.

Dr, Kayumba na Eng, George wakiendelea kutoa mada katika Studio za Bomba fm Mbeya.




Wamiliki wa makampuni na mashirika binafsi mkoani Mbeya wametakiwa kujisajiri  kwa wakala wa afya na usalama mahali pa kazi kutoka katika ofisi ya Wizara ya afya, Occupational  Safety  and  Health Authority  (OSHA).

Kauli hiyo imetolewa na mkaguzi mkuu wa OSHA Tanzania bara Dr, Akwilina Kayumba alipokuwa akiongea na katika kituo cha Radio Bomba fm katika kipindi cha Amka Bomba kinachorushwa kila siku ya jumatatu mpaka ijumaa kuanzia saa kumi na mbili na nusu asubuhi mpaka saa nne asubuhi.

Kayumba amesema kuna makampuni mengi hayajajisajiri na osha, ambapo si sahii kuanzisha kampuni bila pasipo kujisajiri na osha na kwakufanya hivyo ni kutowatendea haki wafanya kazi waliopo katika makampuni hayo.

Aidha Kayumba amesema katika kuelekea katika siku ya maazimisho ya afya na usalama mahali pa kazi kunakila sababu ya makampuni na mashirika ambayo hayajajisajiri na osha ni vizuri yakajisajiri ili kuleta usawa kati waajiri na waajiriwa.

Kwaupande wake Meneja wa osha kanda ya nyanda za juu kusini Eng. George Chali amesema kuna baadhi ya wamiliki wa makapuni wamekuwa wakidhani kusajiriwa na osha ni jambo gumu bali ni jambo jepesi na halina mzunguko mkubwa.

Eng. Chali ameto wito kwa baadhi ya makampuni yasiyosajiriwa kuchukua hatua ya kujisajiri sasa na kwamba siku ya jumamosi kuta kuwa na kikao baina osha na wadau wake wakiwemo wamiliki wa makampuni na wafanyakazi wake katika ofisi za osha jijini Mbeya kuanzia saa nne mpaka saa sita.

Hata hivyo Chali amewataka wadau wa makampuni na wafanyakazi wake kujitokeza kwa wingi ili kuzungumza mambo mbali mbali yanayohusu afya na usalama mahali pa kazi.


                                       Na Lumemo blog.






Post a Comment

 
Top