GuidePedia

0
UTUMIKISHWAJI wa watoto walio chini ya miaka 16 limeibuka wilayani Rungwe mkoani Mbeya baada ya wajasiliamali wanaojishughurisha na biashara ndogondogo wakiwemo wauza nyama za kuchoma(MISHIKAKI) wanaodaiwa kwenda vijijini na kuwarubuni watoto wadogo na kuwatumikishwa katika biashara zao na kuwapa ujira mdogo.

Lumemo Blog hii ilifanya uchunguzi wa siku tatu na kufanikiwa kuwapata watoto 15 waliochini ya miaka 16 na kufanikiwa kufanyanao mazungumzo na kubaini kuwa wapo zaidi ya hao ambao wengi wao walihitimu darasa la saba na kuchaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza na kushidwa kujiunga kutokana na ukosefu wa fedha kwa wa zazi wao.

Mtoto Bonifas Elyud (15) mkazi wa Kasumulu Boda wilayani Kyela alisema kuwa yeye alihitimu darasa la saba katika shule ya msingi Ruangwa na kuchaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika shule ya Kiwira Col mine (KCM) mwaka 2013 lakini alishindwa kujiunga na masomo kutokana na wazazi wao kuishi tofauti baada ya ndoa yao kuvunjika.

Alisema kuwa baba yake anaishi jijini mwanza baada ya kuachana na mama yake ambaye kwa sasa ni mremavu wa macho (Kipofu) anayeishi  na dada yake maeneo ya Bujesi Kijiji cha Ikomelo kata ya busale wilayani kyela huku yeye akiwa hana muelekeo wa maisha pamoja na kuwa alichaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha kwanza katika shule ya sekondari ya KCM.

Aliongeza kuwa baada ya siku kadhaa alikuja kijana mmoja anayeitwa Jeremia Sanga mkazi wa Kata ya Kawetele Rungwe akimuhitaji akafanye kazi ya kuuza mgahawa wake uliopo Tukuyu mjini na kumuahidi kuwa baada ya muda atampeleka shule,lakini amemaliza mwaka akimtumikia bosi wake huyo lakini hakuna dariri zozote za uwepo wa kumpeleka shule huku akiendelea kutumikishwa kwa malipo ya Tsh.1000 kwa siku.

Aliendelea kusema kuwa yeye hana mawasiliano na Baba yake lakini kama kuna msamalia mwema anataka kumsomesha yupo tayari kuingia darasani na kuwa amekuwa hakikosa raha kutokana na umri wake kuwa mdogo huku akifanya kazi ngumu huku watoto wenzake wakiendelea na masomo.

Lumemo Blog hii iliutafuta uongozi wa kata hiyo ya kawetele na kufanikiwa kumpata diwani wa kata hiyo Anyimike Mwasakilali ambaye mbali na kukiri kuwepo na hali hiyo lakini alisikitishwa na kasi ya ongezeko la watoto hao wanaotumikishwa kinyume na sheria huku akiahidi kufanya msaka wa nyumba hadi nyumba ili kuwabaini watoto hao pamoja na kuwachukulia hatua wale wanaowaajiri.

Mwasakilali alisema kuwa katika kata yake wanaoutaratibu wa kuwasajiri watoto yatima walifiwa na wazazi wao na wale waishio katika mazingira magumu ambao wamewasajiri na kuwapeleka shule pamoja na kuwapa  huduma kadhaa za msingi na kuwa uwepo wa watoto hao wanaotumikishwa yeye hana taarifa nao kutokana na kuingizwa katika wilaya hiyo kwa njia za panya.

Aliongeza kuwa kwa kushirikiana na uongozi wa kata na wilaya kwa ujumla watafanya msako utakaoambatana na kuwachukulia hatua watu watakaobainika kuwa ndiyo wanaowaajiri watoto hao ili iwe fundisho kwa wengine wasiokuwa na huruma kwa watoto hao.

Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa asilimia 80 ya watoto wanaotumikishwa wanatoka katika kata ya Busale wilayani Kyela na tayari mawasiliano yamefanyika na uongozi wa kata hiyo ukiongozwa na diwani wa kata hiyo Ezekia Msyani ambaye ameahidi kuanza kulifanyia kazi tatizo hilo.

                                                      Na Lumemo blog

Post a Comment

 
Top