GuidePedia

0


SERIKALI  mkoani Rukwa imewataka  wazazi wanaowakataza vijana wao kwenda kufanyiwa tohara  kwa mwanaume kuacha mara moja kwani huduma hiyo imethibitika kitaalamu kuwa ina faida nyingi  ikiwa ni pamoja na kupunguza uwezekano mkubwa wa kupata maambukizi mapya ya ukimwi kwa asilimia 60

Wito huo umetolewa na mkuu wa wilaya Nkasi Idd Hassan Kimanta kwenye ufunguzi wa kampeni ya tohara kwa wanaume mkoani Rukwa  iliyofanyika katika zahanati ya Chala wilayani Nkasi  ambapo alimwakilisha mkuu wa mkoa Mhandisi stella manyanya ambapo amesema kuwa  tohara ni jibu la kupambana na magonjwa yatokanayo na ngono

Hivyo amewataka wanaume wote ambao bado hawajajitokeza kufanyiwa tohara hiyo kujitokeza na kuitumia fursa hiyo ambayo inapatikana bure kutokana na umuhimu wa kiafya katika kujenga jamii iliyo salama
Pia kimanta amefurahishwa na maendeleo yaliyopo sasa toka zoezi la tohara kuanza katika zahanati ya chala na kwani mpaka sasa wanaume 583 wamejitokeza kufanyiwa toharan ndani ya wiki mbili tu na kudai kuwa kasi hiyo inaleta matumaini makubwa ukilinganisha na agizo la taifa ambalo linataka wanaume 22000 mkoani Rukwa wawe wamefanyiwa tohara na kuwa hadi sasa ni watu 7000 tu na kuwa bado safari ni ndefu

Mganga mkuu wa mkoa Rukwa Dkt,John Gurisha kwa upande wake alisema tohara kwa mwanaume inawasaidia wanandoa wote wawili kuweza kuondokana na matatizo yasiyo kuwa ya lazima kama magonjwa ya kansa ya shingo ya kizazi kwa wanawake,uwezekano wa kupata maambukizi ya virus vya ukimwi kupungua kwa asilimia 60 ikiwa ni pamoja na suala la usafi kwa ujumla

Hivyo alidai kuwa hatarajii kusikia kuwa kuna baadhi ya watu ambao watashindwa kujitokeza kufanyiwa tohara hiyo,lakini pia alionyesha kufurahishwa na kasi ya tohara katika kituo hicho cha Chala kwa maana kuwa kwa siku moja wanaume 150 wanafanyiwa na kuwa kasi hiyo ikiendelea hivyo mkoa Rukwa unaweza ukafanikiwa kwa kiasi kikubwa juu ya tohara hiyo

Zoezi hili lililoanza marchi 17 mwaka huu linatarajia kumalizika marchi 30 na mkoa Rukwa una vituo sita vinavyotekeleza mradi huo wa tohara bure kwa mwanaume chini ya ufadhili wa shirika lisilokuwa la kiserikali la Waterleed Tanzania na vituo ni Chala,Korongwe,Muze,Ilemba,Kapozwa na mkowe ukiachana na vituo vitano tofauti vinavyoendelea na utoaji wa huduma hii ya tohara ambavyo ni Mtowisa,Matai,Nkomolo,Kirando pamoja na kituo mama cha hospitali ya mkoa iliyopo Sumbawanga

                              Na, Lumemo blog

Post a Comment

 
Top