GuidePedia

0


Wananchi wa kata zilizopo liuli,Lupingu,Lumbila,Lifuma,Iwela na Kilondo zilizopo Tarafa ya Mwambao wilayani Ludewa mkoa mpya wa Njombe wameilalamikia Serikali kupitia halmashauri ya wilaya hiyo kwa kushindwa kuwaondolea kero zilizopo katika tarafa hiyo tangu nchi ipate uhuru mwaka 1961 hadi sasa.

Wakizungumza na Lumemo blog wananchi hao  walisema kuwa vijiji vilivyopo kwenye kata hizo vinakabiriwa na changamoto nyingi lakini viongozi wa serikali na halmashauri wameshindwa kuondoa changamoto hizo kwa muda mrefu na kuwa wamepeleka malalamiko yao kwa maandishi juu ya matatizo ya Tarafa hiyo lakini hakuna kinachoendelea.

Dadi mapunda mkazi wa kijiji cha Liunji alisema kuwa Tarafa hiyo ya mwambao inakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo ya ukosefu wa umeme,maji safi,mawasiliano,barabara ,shule,vituo vya afya na uhaba wa watumishi ambao wengi wao hutoroka kufanya kazi mara baada ya kuripoti kutokana na miundombinu mibovu pamoja na ukosefu wa huduma za msingi za kijamii.

Alisema kuwa katika suala la mawasiliano wamekuwa wakipanda juu ya miti na kupanda kwenye mirima mirefu huku wengine wakitembea umbali mrefu kufuata huduma za network hali ambayo inahatarisha maisha yao na kuwa watoto wao pia hutembea umbali mrefu kwenda shule kutokana na kuwa na shule chache huku elimu katika Tarafa hiyo ikizidi kushuka siku hadi siku.

Nyongo Makwaya mkazi wa kijiji cha Ndowa kwa upande wake alisema kuwa Tarafa hiyo ya mwambao imekosa huduma za vituo vya afya vilivyopo havikidhi mahitaji ya wananchi hali inayopelekea watembee umbali mrefu wa kutumia Boti na Mitumbwi kufuata huduma za matibabu katika hospitali ya misheni ya Matema beach na kusababisha baadhi ya wagonjwa kufia njiani kabla hawajafika hospitali kutokana na umbali mrefu.

Alisema kuwa walikwisha andika barua kuiomba halmashauri juu ya kero hizo ili iweze kutafuta tiba ya kutatua tatizo hilo lakini bado hali ni tata na kuwa kama hali itaendelea kuwa hivyo kunauwezekano wa vijana wote ambao ndiyo nguvu kazi ya vijiji hivyo kuyatelekeza makazi hayo na kwenda kuishi sehemu nyingine ambako hakuna changamoto kwa lengo la kutafuta unafuu wa maisha.

Hata hivyo baadhi ya viongozi katika Tarafa hiyo wakiongozwa na Sosten Haule,Chrispin Mwendapole mbali na kukiri kuwepo na tatizo hilo pia walisema kuwa serikali kupitia halmashauri ya wilaya ya Ludewa wanalijua tatizo hilo na wanajipanga ili kujalibu kupunguza changamoto zilizopo.

                             Na, Lumemo blog

Post a Comment

 
Top