GuidePedia

0

Mkuu wa mbeya Mh, Abas Kandoro akiongea neno katika hafla hiyo


Mwenyekiti wa usalama barabarani mkoa wa Mbeya ambaye pia ndio Mkurugenzi wa Kampuni ya Mwaji Group iliyopo uyole jijini Mbeya Allan Mwaigaga akiongea jambo kuhusu hafla hiyo.

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mh, Abas Kandoro na Kamanda wa Polisi Mkoa wa mbeya Ahmed Msangi wakikiwa katika moja kati ya mabasi hayo wakijaribu kukaa katika siti za mabasi hayo.

 

Meza kuu katika hafla hiyo kutoka kushoto wa tatu Mkuu wa mkoa wa mbeya Abas Kandoro na kutoka kulia wa kwanza kamanda wa Polisi Mkoa wa mbeya Ahmed Msang.

                      Hii ni sehemu ya ndani ya mabasi hayo




 Moja kati ya madereva wa mabasi hayo Bi, Nusura Maguluko akiwa ndani basi.

 

 



Madereva mkoani Mbeya kujihadhari na vitendo vinavyoweza kuwapunguzia umakini wawapo safarini ili kuepusha ajali ambazo zimekuwa zikigharimu roho za watanzania wasiokuwa na hatia.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro wakati akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa mabasi ya kisasa ya Ndenjela Jet kuwa tabia ya ulevi, matumizi ya simu wanapoendesha magari, mazungumzo  na mwendo kasi ni vitu vinavyoweza kumpunguzia dereva umakini awapo safarini.

Kandoro amesema pia madereva waache kuyapita magari mengine katika maeneo yasiyoruhusiwa abiria na wamiliki wa magari wakishirikiana wanaweza kutoa mchango mkubwa katika kupunguza ajali nchini

Aidha Kandoro ameongeza kuwa kumekuwapo na madai kutoka kwa madereva kwamba wanaendesha kwa mwendokasi kutokana na kwamba wanalipwa kidogo na wamiliki wa magari sababu ambazo si za msingi sana bali wanapaswa kuwajali abiria wanaokuwa wamewabeba na wao wenyewe.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya Ahmed Msangi akizungumza katika hafla hiyo aliwakumbusha wana Mbeya umuhimu wa kutoa ushirikiano katika kuimarisha ulinzi ili mkoa uendelee kuwa tulivu utakaowavutia wawekezaji.

Awali akizungumza wakati wa kumkaribisha mgeni rasmi mmiliki wa mabasi hayo Allan Mwaigaga amewaasa watanzania kutumia fursa ya mazingira yaliyopo katika kuwekeza ili kuchangia katika kuinua uchumi wan chi kwakuwa hakuna mtu mwingine wa kuja kuwekeza nchini bali ni watanzania wenyewe.

Ameseongeza kuwa magari yanayozinduliwa ni magari ambayo yamesanifiwa hapa nchini ili kukidhi mahitaji ya barabara za Tanzania na kwamba kumwezesha msafiri kujiona kama safari sio kero bali ni sehemu ya kupumzika.


                                 Na, Lumemo blog







Post a Comment

 
Top