GuidePedia

0

Mkuu wa wilaya ya mbeya mjini Dk Norman Sigala akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kampeni hiyo katika ofisi za mkuu wa mkua wa mbeya Mh, mbeya.

Baadhi ya waandishi wa habari mkoani mbeya wakimsikiliza mkuu wa wilaya Dk Norman Sigala.

Mratibu wa huduma za chanjo mkoa wa mbeya Japhet Mhaye akisisitiza  jambo kwa waandishi wa habari.

 

Serikali mkoani mbeya inatarajia kufanya kampeni ya utoaji wa chanjo ya Surua-Rubella kwa watoto wenye umri  kati  ya miezi tisa mpaka miaka kumi na  tano kwa lengo la kudhibiti na kukinga milipuko ya Surua ili kutokomeza ugonjwa huo.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkuu wa wilaya ya mbeya Dk. Norman Sigala kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa mbeya Mh. Abas Kandoro katika ofisi za mkuu wa mkoa huyo amesema serikali ilianzisha mpango wa kufanya kampeni chanjo hiyo tangu mwaka 1999 huku kampeni ya mwisho ilifanyika mwaka 2011 na kampeni ya mwaka huu itaanza tarehe 18 oktoba mapaka tarehe 24 oktoba.

“kuanzia oktoba 18 mpaka oktoba 24 wizara ya Afya na ustawi wa jamii kupitia mpango wa taifa wa chanjo ikishirikiana na wadau wa chanjo itafanya kampeni ya chanjo ya Surua-Rubella kwa watoto wote walio na umri wa kati ya miezi tisa mpaka kumi na tano”  alisema Dk, Sigala.

Dk. Sigala alisema kuwa kampeni hii itahusisha mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar na itaendeshwa katika vituo vya kutolea huduma ya Afya, shule za msingi na sekondari, na vituo maalumu vitakavyoundwa kipindi cha kampeni ili kuongeza huduma karibu na walengwa.

Dk. Sigala alisema licha ya kiwango cha chanjo kuendelea kuwa juu milipuko imekuwa ikitokea kutokana na kuwa watoto takribani asilimia 20kwa baadhi ya wilaya hawapati chanjo.

“ni wazi kuwa watototakribani asilimia 20 kwa baadhi ya wilaya hawapati chanjo na kwa wale waliopata chanjo kwenye umri wa miezi tisa asilimia 15 hawapati kinga kwasababu ya kibailojia katika umri huo, hivyo kampeni ya Surua huwapa watoto ambao hawakupata kinga kwasababu zozote zile, hiyo  ndio fursa nyingine ya kukingwa na ugonjwa hatari wa Surua na Rubella  kwani huu ni mpango wa kidunia wa kutokomeza maradhi ya surua na rubella ifikapo mwaka 2020 hivyo nawaomba wakazi wa mkoa wa mbeya kujitokeza kwa wingi kuwaleta watoto wao ili kukamilisha zoezi hili kwa kiwango kikubwa na kwamba kampeni hiyo kwa mkoa wa mbeya itafanyika katika Halmashari zote kumi na uzinduzi rasmi utafanyika oktoba 18 wilayani Ileje” alisema Dk Sigala.

Aidha Dk Sigala alisema ni kudumisha upunguzaji wa magonjwa, ulemavu na vifo vinavyotokana na surua na rubella, ambapo kampeni hiyo itakwenda sanjari na utoaji wa matone ya vitamini A na dawa ya kukinga ugonjwa wa minyoo, usubi, mabusha, matende, na ngiri maji na kwamba chanjo hiyo itatolewa bure.

Hata hivyo mratibu wa huduma za chanjo mkoa wa mbeya Japhat Mhaye alisema chanjo hiyo inafaida kubwa kwa wananchi kutokana na maradhi yanayojitokeza kwa watoto wanapofikia umri fulani pia amewatoa hofu wananchi kuhusu uwenda chanjo hiyo inamadhara, amesema chanjo hiyo ni salama wala haina madhara yeyote.


                                Na, Lumemo blog




Post a Comment

 
Top