Gari ya askari wa kutuliza ghasia ikiwa katika eneo la tukio na askari wakiwa ndani ya gari hilo.
Wananchi wa kata ya
lwangwa Halmashauri ya Busokelo wilayani Rungwe
mkoani Mbeya wameandamana mpaka katika ofisi za
Halmashauri hiyo wakishiniza serikali wilayani humo kuwatoa watu walio
kamatwa baada ya kuhusiwa kuhusika na kifo
cha Gabriel Mwandemwa mwenye umri wa
mika {40} aliye uwawa na wananchi katika siku
za hivi karibuni kutokana na imani za kishirikina.
Wakizungumza na waandishi wa habari wakati wa mandamano
hayo wanachi hao walisema hatua hiyo
ilikuja kufuatia jeshi la polisi
wilayani humo kuwakamata baadhi ya
wananchi kwa madai ya kuhusika na kifo cha
kijana huyo aliyefariki dunia siku za hivi karibuni kutokana na vitendo
vya ushirikina.
Walisema mnamo majira ya usiku wa
kuamkia oktoba moja jeshi la polisi liliwasili
kinyemela katika maeneo hayo kwa kuwakamata baadhi
ya wananchi bila kushirisha uongozi
wa maeneo husika kwa kufikishwa kituoni, ambapo
hali hiyo ilikupelekea wao kama wanachi
kuchukua hatua ya kupinga kitendo
hicho kwa kuungana kwa pamoja na
kufanya maadamano ya amani hadi katika ofisi ya
mkurugezi wa Halmashauri hiyo wakitaka kutolewa kwa
ndugu zao.
Hata hivyo jeshi la polisi
liliwasili eneo la tukio na
kisha kuanza kusaidia kuzuia ghasia hizo ikiwa ni
pamoja na kuwatia hatiani wale wote ambao
walionekana kuanzisha vurugu hizo.
Diwani wa kata hiyo Robati Mwaibata alikiri kuwapo
kwa adha hiyo na kusema mpaka sasa
wameshindwa kuongea na wananchi wake kutokana
na vurugu kuendelea kuchukua nafasi yake.
Alisema chanzo cha tukio
hilo ni baada ya jeshi la polisi kuwakamata baadhi
ya vijana wa eneo hilo kwa tuhuma za kuhusika na mauji ya Gabriel
Mwandemwa aliye fariki dunia siku za hivi karibuni kwa kukatwa
na mapanga na kisha mwili wake kuchomwa moto.
Alisema mpaka sasa wanaendelea kutuliza ghasia hizo
kwa kushirikiana na jeshi la polisi wilayani
humo .
Hata hivyo juhudi za kumtafuta
mkuu wa wilaya ya rungwe krspini meela ziligonga mwamba mara baada ya simu
yake kuita bila kupokelewa.
Na,
Baraka Lusajo Rungwe
Post a Comment
Post a Comment