GuidePedia

0


WATU watatu akiwemo mwanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari mkoani Mbeya wamefariki dunia wakati wakiogelea katika fukwe za Matema beach katika ziwa nyasa liliopo wilayani Kyela mkoani Mbeya.

Akizungumza na waandishi wa habari mmoja wa shuhuda wa tukio hilo aliyenusurika na maafa hayo Godfrey Richard amesema yeye Akiwa na rafiki zake wawili ambao ni madereva Bodaboda ambao ni Mark Mwakipesile (17) na Noea Noha (16) wakazi wa kijiji cha Kawetele wilayani humo na kumtaja mwingine aliyetambulika kwa jina moja la Happy mkazi wa kijiji cha malindo wilayani humo aliyekuwa anasoma chuo cha uandishi wa habari mkoani Mbeya na kusema  kabla ya  maafa  hayo  aliambatana na wanafunzi wengine mkoani hapa walioenda kuogelea katika ziwa hilo.

Amesema wao hawakujua kuwa ziwa limechafuka waliingia kuoga wakati ziwa likiwa na mawimbi na kuwa yeye alikuwa wa kwanza kukumbwa na kadhia hiyo na baadaye alifanikiwa kijiokoa huku wenzake wakiwa wamezidiwa na  harakati za kuwaokoa ziligonga mwamba.

Amesema wananchi wanaoishi pembezoni mwa ziwa hilo walifika baada ya kusikia mayowe ya kuomba msaada na kufanikiwa kuwatoa watu hao wakati wamekwisha kata roho na kwamba waliwapeleka kuwahifadhi katika hospital ya misheni ya matema beach iliyopo jirani na fukwe hizo na  kuongeza kuwa baada ya hapo taratibu za kuisafirisha miili hiyo ilifanyika na hivi sasa imehifadhiwa katika hospitali Makandana iliyopo wilaya ya Rungwe huku ndugu wa marehemu wakiendelea na maandalizi ya mazishi.

Mwenyekiti wa kitongoji cha kawetele chini Syemu Melele amesema kitenda cha maafa kilichotokea kwa vijana hao kimewasikitisha na kuwa walikwenda kuogelea bila kutoa taarifa kwa wazazi wao na kuwa watafanya mikutano ya kukemea misafara ya kwenda matema beach pasipo kutoa taarifa.

                                  Na, Baraka Lusajo Kyela


Post a Comment

 
Top