GuidePedia

0


SERIKALI ya Kijiji cha Ndaga kata ya Isongole wilayani Rungwe mkoani Mbeya imetumia zaidi ya milioni 90 kujenga miradi ya maendeleo ya kijiji hicho ikiwemo Shule ya msingi,ofisi ya kijiji na vyoo katika soko la kijiji kwa kutumia fedha zao zilizotokana na vyanzo viwili vya mapato vilivyopo kijijini humo.

Akizungumza  kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika jana kwenye viwanja vya ofisi ya kijiji hicho mwenyekiti wa kijiji hicho Paulos Zambi alisema kuwa kijiji chake kinategemea ushuru unaotokana na zao la viazi mviringo na mahindi na katika makusanyo hayo wameamua kujenga miradi ya maendeleo kwa faida ya kijiji na wilaya kwa ujumla ili kuondoa changamoto zilizopo.

Alisema kuwa kwa upande wa shule ya msingi Goye yenye vyuimba sita vya madarasa wametumia Tsh,60.000,000/- kwa mchanganuo ufuatao,Tsh,9,000,000/- zilitokana na harambee,Tsh,7,000,000/-michango ya wanakijiji,Tsh,30,000,000/-miradi ya kijiji na Tsh,14,000,000/-kutoka miradi isiyorasmi ikiwemo adhabu ndogondogo kwa wale walinaokiuka taratibu zilizowekwa na kijiji hicho.

Zambi aliyechaguliwa uenyekiti kwa tiketi ya CUF aliendelea kusema kuwa idadi hiyo ya ujenzi iliyotajwa imejumuishwa pamoja na Tsh,20,000.000/-zilitumika kulipa fidia kwa mtu mwenye eneo palipojengwa shule hiyo na kufikia idadi hiyo ya Mil,60 na kuwa kilichobaki ni kujenga vyoo pamoja na kupiga plasta jingo zima jitihada ambazo tayari wamezianza.

Kwa upande wa ofisi ya Kijiji Mwanyekiti huyo alisema kuwa kijiji hicho kilianza kujenga ofisi hiyo tarehe 2/11/2011 ambapo wametumia Tsh,32,000,000/-ambapo Tsh,11,000,000/-zilitokana na miradi rasmi ya kijiji na Tsh,21,000,000/- zilitokana na miradi isiyorasmi ikiwamo ya adhabu ndogo ndogo kwa wale waliokuwa wakikiuka taratibu zilizowekwa na kijiji.

Aidha mwenyekiti huyo aliongeza kuwa serikali yake ilitumia Tsh,4,500,000/- kujenga choo katika maeneo yanayotumika katika shughuri za kijamii ikiwemo soko la kijiji na Tsh,4,50,000 zimetumika kujenga choo kwenye makao makuu ya kijiji hicho ili kupungunza adha waliyokuwa wakiipata wananchi wa kijiji hicho na jumla ya ujenzi wa vyoo hivyo ni Tsh,9,000,000/- na kuondoa kero zilizokuwepo kijijini hapo kwa fedha zao bila kupata msaada serikalini.

Afisa mtendaji wa kata hiyo Laiponia Mwakisambwe alisema kuwa viongozi wa kijiji hicho kwa kushirikiana na wananchi wameweza kufanya mambo makubwa ya kukamirisha miradi hiyo kwa nguvu zao na kuwa baada ya ujenzi wa shule ya msingi kukamilika wanampango wa kujenga shule ya sekondari ya kijiji siku za usoni ili kuondoa usumbufu wanaoupata wanafunzi wa kutembea umbali mrefu kwenda shule na kuongeza kiwango cha elimu kijijini hapo na kata kwa ujumla.

Afisa elimu msingi wa wilaya ya Rungwe Enock Kyando mbali na kupongeza juhudi hizo zilizofanywa na kijiji hicho alisema kuwa atapeleka waalimu wa kutosha pindi tu viongozi wa kijiji hicho watakapojenga vyoo na kuwa hatua waliyoifanya inapaswa kuigwa na vijiji vingine ambavyo vimekuwa nyuma kufanya maendeleo yakiisubiri serikali ifanye.

Mkuu wa wilaya hiyo Chripin Meela kwa upande wake alimuagiza afisa elimu kuwa ifikapo tarehe 1/1/2015 shule hiyo iweimeanza kupokea wanafunzi na kuwa serikali itaangalia mahali walipokwama ili iweze kusaidia katika harakati hizo za kijiji za kukamirisha miradi hiyo.

Katika mkutano huo ulioambatana na ufunguzi wa miradi hiyo pamoja na sherehe watu mbalimbali na wageni waalikwa walipata nafasi ya kusema ikiwa ni pamoja na kutoa kile walichokuwa nacho ili kusaidia jitihada hizo ambapo fedha taslim Tsh,9,26,400 zilipatikana pamoja na mifuko 79 ya saruji yenye thamani ya Tsh,mil 1,3,43,000/-.


                                       Na, Lumemo blog

Post a Comment

 
Top