GuidePedia

0


MAHAKAMA ya wilaya Nkasi mkoani Rukwa  imemhukumu kwenda jela miaka 30 Martin Misala (20) mkazi wa kijiji cha Katongolo kata ya Kipili wilayani Nkasi kwa kosa la kumbaka mtoto mwenye umri wa miaka (16) na kumsababishia maumivu makali

Akitoa hukumu hiyo hakimu mfawidhi wa mahakama ya wilaya Nkasi Ramadhan Rugemalila alisema kuwa anamtia hatiani mtuhumiwa baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka pasipo kuacha shaka yoyote na kuwa anamtia hatiani kwa kosa hilo la ubakaji chini ya kifungu cha sheria No,130(1)(2)

Upande wa mashitaka ukiongozwa na mwendesha mashitaka wa jeshi la polisi Hamimu Gwelo uliiambia mahakama hiyo kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo la kumbaka binti huyo oktoba (20) mwaka jana majira ya saa 6 usiku katika kijiji hicho cha Katongolo walipokua wametokea disko.

Katika kesi hiyo upande wa mashitaka uliitisha mashahidi wanne ambao walitoa ushahidi wao huku mtuhumiwa akikosa watu wa kumtetea na ndipo mahakama ilipoamua kumtia hatiani kwa kosa hilo baada ya kuridhishwa na maelezo yaliyotolewa na upande wa mashitaka

Kutokana na kosa hilo upande wa mashitaka uliiomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali kwa mtuhumiwa huyo ili liwe ni fundisho na kwa wengine baada ya vitendo kama hivyo kushamiri wilayani Nkasi katika siku za hivi karibuni

Mtuhumiwa kwa upande wake aliiomba mahakama hiyo kumpunguzia adhabu kwa sababu yeye hilo ni kosa lake la kwanza lakini pia familia yake inamtegemea sana

Wakati huohuo mahakama hiyo imemhukumu kwenda jela miaka 15 Masanja Lupinga mkazi wa kijiji cha Katani kwa kosa la uwizi wa ng’ombe.

Upande wa mashitaka uliieleza mahakama hiyo kuwa septemba 16 mwaka jana mtuhumiwa huyo aliiba ng’ombe 8 za Lauliano Kayoka mkazi wa kijiji cha Ntemba

Alisema ngombe hao walikamatwa mjini Sumbawanga pamoja mtuhumiwa huyo wakizipeleka machinjioni kwa ajiri ya kwenda kuwauza

Upande wa mashitaka uliita mashahidi 8 wakiwemo na ng’ombe hao kama kielelezo mahakamani na kwa kuzingatia kuwa mtuhumiwa hili si kosa lake la kwanza mahakama hiyo ilimtia hatiani kwenda kutumikia kifungo cha miaka 15 jela chini ya kifungu No,168 na 165 ya kanuni ya adhabu sura ya 16.


                                            Na Lumemo blog

Post a Comment

 
Top