GuidePedia

0





Baadhi ya mizigo ya anayetuhumiwa imani za kishirikina ikitokewa nje na wafanyakazi wenzie.


Wafanyakazi wa  kiwanda cha  chai  chivanje    katika  kijiji cha  Itula   kata  ya itula  Wilayani  rungwe  mkoani  mbeya  wamemtuhumu mfanyakazi mwenzao kwa imani za kishirikina Faustina Sakogo na kumfukuza   katika kambi wanayoishi na kudai  ameleta  ugonjwa wa kuhara katika kambi yao.
Wakiongea na waandishi wa habari katika mkutano wa  hadhara kijiji hapo  wamesema  chanzo  cha  tukio hilo   ni baada ya mama  huyo   kuleta ugonjwa  wa kuhara  kambini  hapo  na kwamba  katika  siku  za  hivi karibuni mama huyo alileta  mchele  ambao alikuwa akiwakopesha   wafanyakazi wenzake   lakini  watu wote ambao walikuwa  wakitumia mchele huo walikuwa  wakihara.
Baada ya mama  huyo kuonyesha ubishi juu  ya suala  hilo ambapo bila kujua aliweza kuingia katika wakati mgumu  baada  ya wafanyakazi hao  kuandamana hadi katika kambi  ambalo alikuwa akishi  na   kwa kutoa mizigo  yake  huku  wakimtaka  aondoke 

Aidha baada ya tukio hilo Faustina Sakogo aliamua   kutoa  taarifa kwa kiongozi wa kiwanda  hicho  Daniel Mwang’ombola ambaye  alifika  kambini  hapo  kwa kuwataka  wafanyakazi  hao kuachana  na  vitendo  vya kujichukulia sheria mkononi.

Baada ya kiongozi  huyo kuondoka  katika  eneo la  tukio  wafanyakazi hao waliamua kuanzisha suala  hilo  upya kwa   kumtaka Faustina  kuondoka  mara moja kiwandani  hapo kabla ya  jua kuzama  ikiwa ni pamoja na  kutoa mizigo yake nje.


                                           Na, lumemo blog


Post a Comment

 
Top