GuidePedia

0


MGOGOLO mkubwa kati ya wavuvi wa forodha ya kafyofyo na wananchi wa kitongoji cha Njisi Kijiji cha Kirwa Kata ya Kajunjumele wilayani Kyela mkoani Mbeya umeibuka na kupelekea hali ya uvunjifu wa amani na umwagaji damu kutaka kutopkea baada ya kutoelewana baina ya watu hao.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye forodha hiyo,Mwenyekiti wa forodha John Ndewele alisema kuwa mgogoro huo ulianza miezi kadhaa iliyopita kwa viongozi wa kijiji cha kilwa kutowatambua huku wakidai kuwa wavuvi hao hawatoi michango ya ujenzi wa miradi ya maendeleo pamoja na kutoshiriki katika shughuri za maendeleo.

Alisema asilimia 80 ya wavuvi katika forodha hiyo ambayo ni kubwa kuliko zote wilayani humo ni kutoka tarafa ya mwambao wilayani Ludewa ambao wapo zaidi ya 50 wanaofanya shughuri za uvuvi katika forodha hiyo iliyopo katika kitongojin cha njisi kijiji cha Kirwa kwa kufuata taratibu zote za idara ya maliasili na uvuvi.

Alisema kuwa baadhi ya wananchi pamoja na viongozi wa kijiji hicho wamekuwa na wivu wa kimasilahi na wavuvi kutokana na wavuvi kutoka wilaya ya Ludewa kuwazidi wazawa kipato cha majini hadi kufikia hatua ya kuwatafutia tuhuma za kuwatuhumu kuwa hawashiriki katika shughuri za maendeleo,wanatembea na wake zao  na kutoa lugha za matusi wa wazawa kitu ambacho si kweli.

Ndewele aliongeza kuwa kitu kitu kinachowauma zaidi ni kutokana na wao kuchukua ubia na halmashauri ya wilaya hiyo kutoza ushuru ambapo kila nyavu ikiingia kuvua inatozwa Tsh,1000 huku mnunuzi utozwa Tsh,500 kila mmoja huku idadi ya nyavu zikiwa 53 na wanunuzi wanaofika kununua samaki ni zaidi ya 200.

Alisema kuwa wao kama wavuvi wapo kisheria na wamekuwa wakilipa zaidi ya mil,6 kwa ajili ya leseni za nyavu pamoja na mitunbwi,ambapo nyavu moja inakuwa na wavuvi 5 mitumbwi 3 katika usajili hutoa Tsh,120,000,yaani nyavu 80,000 mtumbwi mmoja 32,000 mvuvi mmoja 7500 mbali na ushuru wa mtu mmoja mmoja na adhabu mbalimbali huku kijiji kikipewa 150.000 kwa mwaka kama ruzuku.

Baada ya kutokea kwa mgogoro huo viongozi wa forodha walipeleka malalamiko kwa mkuu wa wilaya Magret Marenga ambaye naye alimtuma Afisa Tarafa wa unyakyusa Hery William ambaye tar,8/5/2014 alifika kijijini humo na kufanya mkutano wa pamoja na kusikiliza pande zote mbili huku kijiji kikitaka wavuvi hao wavunje makambi uwepo mwalo na wao waishi uraiani ili waweze kushirikiana katika shughuri za maendeleo.

Alisema afisa huyo aliwaeleza wananchi kuwa wawape mwezi mmoja siku ya tar,8/6/2014 ili wavuvi hao waweze kujipanga zaidi kuliko kutoa amri ya kuwaondoa maeneo hao kighafra wakati hawana maeneo mengine ya kuishi zaidi ya kambini,na kuwa siku hiyo muafaka wa jambo hilo haukufikiwa huku wao wakiendelea kuishi katika makambi hayo na kupokea vitisho kutoka kwa wanakijiji hao.

Mwenyekiti wa kitongoji hicho cha njisi Ndenge Mwakilasa alikiri kuwepo na mgogoro huo na kudai kuwa wavuvi hao wamekuwa hawashiriki katika shughuri za maendeleo huku wakidai kuwa wao wapo chini ya maliasili na si Kijiji kitu ambacho kimeleta utata na kuwa walifanya mikutano ya kuwataka waishi vijijini huku ziwani wawe wanaenda kuvua na kurudi na si kweka makambi kitu ambacho wao wanakipinga.

Mwenye kiti wa kijiji cha Kilwa Padon Mwangwala kwa upande wake alidai kuwa uongozi wa kijiji chake ulipokea muhtasari wa kikao cha kitongoji kikitaka wavuvi hao wahamie vijijini na kuvunja makambi na wao kupeleka kwenye kata na kukaa vikao vya (WDC) na kupeleka muhtasari kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya ambayo ilitoa tamko katika mkutano kuwa ifikapo tar.8/6/2014 wavuvi wawe wamehamia vijijini.

Alisema wao wakiwa wanasubiri tarehe hiyo walishangaa kuona mkuu wa wilaya ya Kyela Magreti malenga siku ya tar,6/6/2014 akienda kwa wavuvi na kuwaeleza kuwa wasiondoke badara ya kuitisha mkutano wa pande zote mbili ili atatue mgogoro yeye ndiyo kachochea mgogoro na kutuzarau sisi ambao ndiyo viongozi wa sehemu husika.

Aliongeza kuwa ilipofika tar,7/6/2014 jeshi la polisi wilayani lilifika kijijini humo na kumkamata Nickson Mwakasonda kwa madai kuwa amefunga barabara ya kutoka kwake kwenda ziwani wakati njia hiyo imepita katikati ya mji wake nay eye aliamua kuifunga ili apande migomba,na hadi sasa kijana huyo yupo lumande.

Kutokana na hali hiyo viongozi wa kijiji hicho wametishia kujiuzuru nyadhifa zao kwa madai kuwa hawatendewi haki,na katika sekeseke hilo zaidi ya wavuvi 100 kutoka wilayani Ludewa wameondoka maeneo hayo wakihofia usalama wao.

Afisa maliasili uvuvi na utalii wilayani Kyela Fedinand  Mwaseba aligoma kulizungumzia sakata hilo na kudai kuwa lipo chini ya mkuu wa wilaya,huku mkuu wa wilaya Magret malenga hakuweza kupatikana ofisini kwake kutokana na kuwa katika mapumziko mafupi na alipo pigiwa simu yake haikupatikana.

                           Na, Lumemo blog

Post a Comment

 
Top