Mjumbe wa baraza la
kuu la taifa kupitia chama cha Chadema
John mwambigija amewataka
wanachi kuwa makini na baadhi ya watu
ambao wamekwa wakizunguka kwa
kueneza kashifa mbaya juu ya chama
hicho.
Hayo yamejili wakati wa
kikao maalumu na waandishi wa habari ambapo amesema kuna baadhi ya watu
wamekuwa wakizunguka katika sehemu mbali mbali nchini kwa
kutoa kashifa mbaya
kwa wananchi kwamba chama cha chadema kinamatumizi mabaya ya fedha jambo
ambalo siyo la kweli.
Amesema mpaka sasa wamejipanga kuzunguka katika maeneo tofauti mkoani
hapa kwakuwakamata watu hao kwa lengo
la kuweza kuwafisha katika vyombo vya kisheria.
Amesema katika kuhakikisha chama
hicho kinasonga mbele
wamefanikiwa kununua magari na
pikipi ambayo mpaka sasa
yanaendelea kutumika nchi nzima kwa
matumizi ya chama husika
na kusema luzuku imeendelea
kufanya kazi yake vizuri bila
kufanya ubadhilifu wowote na viongozi
husika.
Kwa upande katibu mwenezi wa chadema mbeya mjini Baraka
Mwakyabula amesema kuhusu uchaguzi wa diwani katika kata ya Ntembela chadema
imejipanga kuhakikisha chama chao kinashinda kwaasilimia mia.
Hata hivyo ametoa angalizo kwa chama cha mapindizi ccm kuacha
vitendo vya kuchakachua matokeo kwani wao wamejipanga vyakutosho juu ya
uchaguzi huo.
Na, Lumemo blog
Post a Comment
Post a Comment