GuidePedia

0
MKAZI wa kijiji cha Kandete kata ya Kandete katika halmashauri ya Busokelo wilayani.Rungwe Mbeya Suzana Osea (25) amejikuta katika wakati mgumu baada ya kuolewa na wanaume wawili na kuzua tafrani kijijini humo.

Akizungumza na   kituo hiki  jana Omari Njela mbaye ndiye anayedaiwa kuwa ni mume halali wa mwanamke huyo alisema alimuoa mwanamke huyo miaka miwili iliyopita na tayari amezaa naye mtoto mwenye umri wa miezi mitatu.

Alisema wiki iliyopita binti huyo alimtelekeza mtoto ndani kwa siku mzima na kufunga mlango kwa nje kasha kuchukua uamuzi mgumu wa kuolewa na mwanaume mungine huku akijua kuwa yeye ni mke wa mtu na kuwa wakati kitendo hicho kinafanyika yeye alikuwa safarini.

Alisema baada ya mtoto kufungiwa mlango alianza kulia kwa uchungu na ndipo majirani waliposhituka na kulazimika kuvunja mlango na kuingia ndani kasha kumkabidhi mtoto huyo kwenye serikali ya kijiji hicho kupitia kwa afisa mtendaji wa kata.

Afisa mtendaji wa kata ya Kandete Huruma Mwakyusa mbali na kukiri ofisi yake kumpokea mtoto huyo alidai kuwa aliamuru wanaume wote pamoja na mwanamke wakamatwe na baada ya kukamatwa serikali ya kijiji hicho kiliketi na kutafuta ufumbuzi wa suala hilo.

Aliongeza kuwa katika shauri hilo mwanamke huyo alishindwa kumtambua mwenye uhalali na mtoto huyo na kuwa ilionekena alikuwa akijivinjari na wanaume wote kwa nyakati tofauti hivyo kuto tambua baba halali wa mtoto.

Kwa upande wake mwanamke huyo alisema alichukua maamuzi ya kuolewa na mume mungine baada ya kuona mumewe amekuwa akichepuka na mwanamke mungine na kufikia hatua kumpangia chumba na kuwa aliamua kufanya hivyo ili kumkomoa.

“mume wangu alipo pata mchepuko huo alianza kunidharau na kuniambia kuwa mimi sina hadhi ya kuwa naye huku akipunguza penzi kwangu ndipo nikachukua maamuzi magumu ya kuamua  kuchepuka na hatimaye kuolewa”alisema mwanamke huyo.

Serikali ya kijiji hicho kilishindwa kufikia tamati ya suala hilo baada ya mwanamke huyo kuwa na msimamo wa kuwa atawamudu wanaume wote wawili alidai ananguvu za kutosha na kuahidi kuwa mwaminifu kwa wanaume hao hadi siku ya kufa.

Kwa upande wao wanaume hao waliafikiana kushea penzi na mwanamke huyo ambapo walipangiana zamu na kutokomea katika kikao hicho huku mamia waliokuwepo kwenye shauri hilo wakishikwa na butwaa kutokana na maamuzi ya wanaume hao kuoa mke mmoja.


                               Na, Baraka Lusajo Rungwe

Post a Comment

 
Top