GuidePedia

0


BODI ya mikopo ya serikali za mitaa hapa nchini imeufanyia marekebisho muundo wake na kutengeneza muundo wa kibenki ambao umeonekana kupendwa zaidi na  wadau wengi kwa kuwa  unaruhusu kuwekeza na kuchangia mtaji kwa njia ya hisa na mikopo kutokana na misingi ya usimamizi na uendeshaji wake ambayo ipo wazi.

Akizungumza na madiwani wa halmashauri ya wilaya Nkasi mkoani Rukwa mjumbe wa bodi hiyo ya mikopo ya serikali za mitaa George malima Lubeleje alisema kuwa chombo hicho ni muhimu sana kwa serikali za mitaa hivyo ni matarajio makubwa kwao kuwa marekebisho ya muundo huo wa bodi ni kuwa  na chombo makini cha kifedha kitakachoziwezesha halmashauri hapa nchini kuendeleza miradi mbalimbali kwa kuwa na uhakika wa kifedha.

Alisema kuwepo kwa benki hiyo ya serikali za mitaa kutapelekea  kuwepo kwa mtaji wa kutosha kukidhi mahitaji ya wakopaji,kuzifanya halmashauri za wilaya kuendeshwa kama kampuni ya kibiasshara(Business entities),kuwafanya viongozi katika mamlaka za serikali za mitaa kuwa na mwamko zaidi wa kuibua shughuli za maendeleo katika maeneo yao,kuongezeka kwa miukopo na viwango vya fedha kuongezeka

Lubeleje alisema kuwa lengo  la serikali   la kufanya marekebisho ya muundo ni kutaka kuwa na chombo cha  fedha cha serikali za mitaa kilichoimarika katika Nyanja tofauti za kiutumishi katika Nyanja  mbalimbali za kiutaalamu,kifedha  na katika technolojia ya habari na mawasiliano,kuwa na chombo kinachojitegemea kwa kuwa na uwezo kiutendaji wa kusimamia na kuendesha shughuli zake kwa asilimia 100 ikiwa ni pamoja na kuwa na uwezo wa kukidhi mahitaji ya mikopo katika ngazi zote za mamlaka ya serikali za mitaa.

Mjumbe huyo wa bodi alifafanua kuwa licha ya hayo yanayofanywa na bodi hiyo ya mikopo halmashauri kwa upande wake zina wajibu  wa kuhakikisha zinasaidia katika kuimarisha bodi ili itoe huduma kwa ufanisi zaidi na kutoa michango kwenye bodi ya mikopo kwa mujibu wa sheria ikiwa ni pamoja na kuirejesha mikopo kwa wakati

Madiwani kwa upande wao walionyesha kufurahishwa na chombo hicho na kudai kuwa wao kama halmashauri hawakukifahamu na kuwa kama bodi hiyo ikitumiwa vizuri kuna uwezekano mkubwa wa halmashauri yao kupiga hatua kubwa katika suala la kujiletea maendeleo

Diwani wa kata ya Nkomolo Sospeter Kasawanga  alisema kuwa wao kama madiwani hawakuitambua bodi hiyo ya mikopo katika serikali za mitaa na kuwa sasa watabaki kujadili kwa kina suala hilo na kujiridhisha kama wanao uwezo wa kukopa na kurejesha mikopo kwa wakati kupitia mapato yao ya ndani.

Mwenyekiti wa halmashauri  ya wilaya  Peter Mizinga kwa upande wake  alisema kuwa halmashauri sasa itajipanga vizuri ili iweze kuona ni namna gani wanavyoweza kuitumia  bodi hiyo katika kujiletea shughuli mbalimbali za kimaendeleo kupitia fursa zilizopo kwenye  bodi hiyo ya mikopo.


                                 Na, Lumemo blog

Post a Comment

 
Top