GuidePedia

0

Mwenyekiti wa kamati ya usalama barabarani mkoa wa mbeya, Allan Mwaigaga akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.


Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mwenyekiti huyo wa kamati ya usalama barabarani mkoa wa mbeya.


Mwenyekiti wa kamati ya usalama barabarani mkoa wa mbeya Allan Mwaigaga amewataka madereva kuwa makini pindi wawapo barabarani kwa lengo la kuepuka ajali zisizokuwa za lazima.

Kauli hiyo ameitoa jana alipokuwa akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake kufuatia ajali zilizotokea mfululizo hivi karibuni ikiwemo ajali ya basi la abiria iliotokea juzi mlima nyoka jijini mbeya.

Mwaigaga amesema asilimia kubwa ya ajali zinazotokea zinasababishwa na makosa ya kibinadamu ambayo yanaweza kuepukika ili hali madereva wakiwa makini na kuzingatia sheria za barabarani.

Aidha Mwenyekiti huyo amesema kumekuwa na imani potofu ya baadhi ya watu kuhisi kuwa wamiliki ndio wanaosababisha ajali kwa madai ya kutoa kafara jambo hilo si la kweli.

“kuna baadhi ya watu wanadhani kuwa kuna uhusiano kati ya ajali zinazotokea na wamiliki pamoja na kuhisi kuwa inapofika mwisho wa mwaka ndio ajali nyingi hutokea jambo hilo sio la kweli hata kidogo bali ni  uzembe wa madereva na kuhusu kuongezeka kwa ajali mwisho wa mwaka  ikumbukwe kuwa mwisho wa mwaka kunaambatana na sikuku hiyo madereva wengi wanatumia nafasi hiyo kuendesa huku wakiwa wamelewa, hivyo nawaasa madereva waache tabia ya ulevi pindi wawapo barabarani” alisema Mwaigaga.

Mwaigaga aliongeza kuwa licha ya kuelekea kipindi  cha sikuku pia kipindi hiki mvua ndio zimeanza hivyo barabara zinakuwa sio nzuri kutokana na mvua kunyesha mara kwa mara.

Na kuhusu ongezeko la ajali Mwenyekiti huyo amesema takwimu za kitaifa zinaonesha ajali zimepungua japo si kwa kiwango kikubwa lakini anaamini elimu wanayoendelea kuto kwa madereva na abiria ajali itazidi kupungua zaidi kwa kumekuwa na ukosefu wa elimu ya usalanma barabarani.

Pia amewataka wamiliki wa vyuo vya udereva nchini kuelekeza sana elimu ya usalama barabarani kwa wanaojifunza masuala ya udereva.

Hata hivyo Mwaigaga amesema matatyizo mengine yanachangiwa na wamiliki wa vyombo vya moto bandia ambao hawatakikujitokeza katika vyama vya wamiliki wa vyombo vya moto ili kupeana elimu juu ya umiliki na jinsi ya kuwabana madereva ambao si waadilifu, hivyo ametoa wito kwa wamiliki wote ambao hawajajiunga katika vyama vya wamiliki wa vyombo vya moto wajitokeze ili kushirikiana kwa pamoja na kuwabana madereva hao ambao wanasababisha ajali zisizo za lazima.

                             Na, Lumemo blog


Post a Comment

 
Top