GuidePedia

0


Katika jitihada za kuongeza  kiwango cha ufaulu  kwa wanafunzi wa shule  za msingi  na sekondari  mkoani hapa , hivyo   walimu wa shule  hizo   wameshauliwa   kuwa na ushilikiano  kwa   kufanya kazi   kwa  pamoja   kwa lengo la  kuongeza  viwango vya ufaulu kwa  wanafunzi  wote.

Hayo yamesemwa  na  afisa maendeleo ya jamii  katika  halmashauli ya busokelo  wilayani  rungwe mkoani mbeya  Agnes elikunda   wakati   uzinduzi  wa maadhimisho ya sherehe ya wiki ya elimu iliyo fanyikia katika  viwanja vya shule ya msingi  lugombo  wilayani hapa .

Ambapo  amesema  ili wanafunzi waendelee kufanya vizuri katika masomo  yao   hivyo walimu na wanafunzi hawanabudi kuchukua hatua ya kushirikiana kwa pamoja   kwa kuwa na wivu  katika  kushindana kimasomo  kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia  kiwango cha elimu kuendelea  kusonga mbele  wakati wote.

Hata  hivyo   elikunda   ametumia fulsa hiyo  kuwataka wanafunzi  wote katika  halmashaul hiyo juu ya kuepukana na vishawishi ambavyo vinaweza kuhatarsha  kupunguza  kiwango cha masomo yao.

Kwa upande  wa  walimu wakuu katika halmshauli hiyo  akiwemo JERMIAH ELESONI KAPANGA  na  Tumparege  mwaibingila wamesema ili kuboresha  elimu katika halmshauli hiyo serikali haina budi kuchukua hatua ya kuboresha  vifaa vya ufundishaji  pamoja na  miundo mbinu  ya shule kama   nyumba za walimu , na vyombo vya ufundi  kwa  fani ya useremala.

Wamesema  endapo  vitu  hivyo vikitatuliwa mapema ufanisi  wa ufundishaji  kwa walimu utaongezeka kwa kiwango cha juu  ikiwa ni pamoja na ufaulu  wa  wanafunzi  kuongezeka  kwa asilimisa kubwa ukizingatia na hapo awari.

 Uzinduzi wa wiki ya elimu katika halmashauli ya busokelo umefanyikia katika  shule ya  msingi ya  Lugombo  ambayo ni miongoni mwa shule iliyo ongoza  katika matokeo ya darasa la saba ikifuatiwa na shule ya msingi  Kisalala.

Post a Comment

 
Top