GuidePedia

0

Afisa Mtendaji wa kijiji Malamba Emmanuel Wiliamu Gwimile, aliyesimama akifungua mkutano.

Mtendaji wa kijiji wa kata ya Rwiwa Zephania Mgaya aliyesimama akielezea baadehi ya changamoto wanakabiliana kwa lengo la kuzimaliza kaqtika kata hiyo.

Mwenyekiti wa kijiji cha malamba Nasibu Edson aliyesimama akizungumzia baadhi ya kero zilizopo katika kijiji hicho.

Diwani wa kata ya Rwiwa Alex Mdimilaje akihutubia kat.ika mkutano huo

B, Shali Kayeto mkazi wa kijiji cha malamba akiuliza swali katika mkutano.

 Baadhi ya wananchi wakisikiliza mkutano katika kijiji cha malamba.




Wananchi wa kijiji cha malamba kata ya wimba  wilaya ya Mbarali vijijini wametakiwa kuacha tabia ya kutowapeleka watoto wao shule ya awali pamoja na darasa la kwanza.

Kauli hiyo imetolewa na Diwani wa kata hiyo Mh, Alex Mdimilaje alipokuwa katika ziara yake ya kuangalia miradi ya maendeleo pamoja na kuwaeleza baadhi ya ahadi zake alizozitekeleza katika kata hiyo.

Mdimilaje amesema kuwa kumekuwa tabia ya baadhi ya wazazi kutowapeleka watoto wao shule badala yake wamekuwa wakiwaacha nyumbani na kuishia kufanya michezo isiyo na tija.

Aidha amesema faida ya kuwapeleka  watoto shule ni kukupa fursa mzazi kufanya kazi za kimaendeleo pasipo kusumbuliwa na watoto hao kani walimu watakao kuwa wanawafundisha wanataaluma ya kuishi na watoto.

Alex Mdimilaje ameongeza kuwa kuna mradi wa umeme unaotarajiwa kuanza hivi punde na tayari fandi wameshaanza kufunya uchunguzi wa kina ili kubani gharama ya kufikisha umeme huo katika kijiji hichi.

Hata hivyo amesema katika kipindi cha uongozi waake mpaka sasa amejitahidi kukamilisha miradi ya kimaendeleo kwa asilimia kubwa tofauti na vile alivyoikuta wakati anaingia madarakani.

Kwa upande wake mtendaji wa kata hiyo Zephania Mgaya amesema serikali inajitahidi kuongezza bnguvu katika miradi hiyo ya maendeleo.

Aidha Mgaya amewataka wananchi kuwa na imani serikali yao pamoja na kutekeleza maagizo yake yakiwemo ya kujiandikisha majina kwaajili ya kupatiwa mashamba ya kulima mazao yatakayowakwamua kiuchumi.

Hata hivyo Mgaya amesisitiza suala la kujikinga na maambukizzi ya UKIMWI kwani ni ugonjwa ambao unamadhara makubwa kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.

                                     Na, Lumemo blog.








Post a Comment

 
Top