baadhi ya viongozi wa kamati hiyo pamoja na viongozi wengine wa kijiji wakiwa meza kuu katika mkutano huo.
baadhi ya wananchi wakiwa katika mkutano huo
baadhi ya wajumbe wakionesha karatasi mbali mbali zinazohusu tuhuma hizo.
Hii ni moja kati ya bili ya maji zilizolipwa na wananchi.
Hii ni hati ya kukiri ya viongozi hao wa badhirifu wa kamati hiyo, kuhusu kutumia fedha kwa manufaa yao binafsi.
Kamati ya maji ya kijiji cha Iwanga Kata ya Utengule Usongwe
Wilaya ya Mbeya inatuhumiwa kwa ubadhilifu wa fedha za mradi wa maji zaidi ya
shilingi milioni mbili zilizochangwa na wananchi wa kijiji hicho.
Tuhuma hiyo imebainishwa na Tume ya Uchunguzi iliyoundwa na
wananchi wa kijiji hicho baada ya kuitishwa mkutano wa hadhara hivi karibuni.
Wanaotuhumiwa kwa ubadhilifu huo ni pamoja na Semu Jaton,Enitha
Mathayo,Daud Mwampashi,Langton Mwawayo na Makala Mwakalemba.
Mwenyekiti wa Tume ya
Uchunguzi Grace Jerema amesema kuwa baadhi ya viongozi wa kamati hiyo
walichukua fedha benki katika akiba ya mradi wa maji kwa matumizi yao binafsi
bila ridhaa ya wananchi.
Jerema amesema Tume yake imebaini mnamo Septemba 19,mwaka
2012 Semu Jaton kwa kushirikiana na Anitha Marijani walichota shilingi elfu
sitini kutoka Benki ya NMB,Desemba 12 mwaka 2012 walichota shilingi laki moja
ambazo pia walitumia kwa matumizi yao binafsi.
Baada ya kubanwa na wananchi walikiri kuchota pesa hizo bila
ridhaa ya wananchi na kuamua kuzirejesha benki, hivyo wananchi kukosa imani na
kamati kwa vile Mwenyekiti wa kamati Julius Mwendo na Mtunza Hazina Christina
Mpunga hawakushirikishwa kwa kuwa wao hawana saini zao Benki.
Kamati ya uchunguzi pia ilibaini kuwa baadhi ya fedha
nyingine zilizokusanywa zilichotwa na Viongozi wa Serikali ya Kijiji akiwemo
Mwenyekiti Aleck Mwasubila aliyedaiwa kujichukulia shilingi laki nne na
ishirini elfu,Mtendaji Kata aliyehamishwa Lwitiko Mwaibindi ,Mafundi Bomba
Lington Mwalingo anayedaiwa kuchota laki moja tisini na nane elfu na Makala
Mwakalemba aliyetafuna shilingi elfu hamsini na mbili ambao wote walitajwa katika
Tume ya Uchunguzi.
Mbali ya tuhuma hizo Tume imebaini kuwa kuna vitabu
vilivyokuwa vinatumiwa na Uongozi wa Kijiji bila kushirikisha Kamati ya maji
hali inayotia shaka kama fedha za maji zilitumika kama ilivyoazimiwa katika
vikao.
Tume ilipokamilisha uchunguzi wake ilikabidhi nakala ya
taarifa ya uchunguzi kwa uongozi wa kijiji na kuomba kuitishwa mkutano Mkuu wa
kijiji ili taarifa hiyo isomwe mbele ya wananchi lakini kulitokea marumbano
baina ya Tume na Serikali kwani Serikali ikitaka kupatiwa nakala halisi.
Aidha Kamati ya Uchunguzi ilisita kukabidhi nakala halisi
Serikalini kwa kuhofu kuhujumiwa hivyo kuomba ipelekwe ofisi ya Mkurugenzi wa
Halmashauri ya Wilaya ili ukaguzi ufanyike na watakaobainika wachukuliwe hatua
za kisheria.
Kutokana na marumbano hayo vikao viwili viliitishwa bila
mafanikio kijijini hapo na kulazimu uongozi wa Kata kuamua kuitisha kikao
kingine Februari 26 mwaka huu kupitia kwa Afisa Maendeleo ya Jamii Kata Martin
Gowele ambaye pia ni Kaimu Afisa Mtendaji Kata ili kulipatia ufumbuzi suala
hilo.
Katika mkutano uliofanyika kijijini hapo Gowele aliagiza kuwa
Kamati ya Uchunguzi ivunjwe na kukabidhi nyaraka zote vikiwemo vitabu vya
kukusanyia fedha ili kazi ya makusanyo iendelee kama awali kupitia mradi wa
maji.
Na, Ezekiel Kamanga
Lumemo blog
Post a Comment
Post a Comment