GuidePedia

0


MAITI 6 kati ya 8 waliofia majini katika ziwa Tanganyika baada ya boti mbili kugongana julai 7 mwaka huu katika kata ya Korongwe wilayani Nkasi mkoani Rukwa zimepatikana huku jitihada za kutafuta miili mingine ikiendelea.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake katibu tawala wa wilaya Nkasi mkoani Rukwa (DAS)Festo Chonya amesema toka boti  hizo zigongane julai 7 kati ya boti ya abiria na ile ya wavuvi na kupelekea boti ya abiria kuzama  watu nane walifia majini na jitihada zilifanywa za kuanza kuitafuta miili hiyo ambapo mpaka hivi sasa ni miili 6 ndiyo iliyopatikanika.

Alisema kutokana na kuwa miili ya watu hao ilikua imeharibika sana serikali ilikataa kusafirisha maiti na badala yake serikali imetenga eneo maalumu katika kijiji cha Korongwe ambapo miili yote iliyopatikana imezikwa  katika kijiji hicho cha Korongwe.

Katibu tawala huyo wa wilaya ametaja majina ya maiti ambao wamepatikana hadi hivi sasa kuwa ni ya Fatuma Masud (46) mkazi wa Mwanza ambaye alikua ni mfanyabiashara,Cleophas  Mwanandenje (47) mkazi wa Kijiji cha Korongwe na mtoto Edward Kangeme (8) mkazi wa kijiji hicho cha Korongwe wilayani Nkasi.

Wengine ni  Anastazia Alex (7) wa Korongwe,Emmanuel Manyika (28) mkazi wa Mpege na Beneth Kasomo (54) wa mkazi wa Challa na kuwa jitihada za kuitafuta miili ya watu wawili waliokufa katika ajali hiyo inaendelea.

Chonya alifafanua kuwa ajali hiyo ilitokea usiku wa tarehe 7 mwezi huu majira ya saa 3 usiku ambapo boti ya abiria iliyokua imetokea katika kata ya kirando walipogongana na boti la wavuvi iliyopelekea boti la abiria kupasuka na kuzama na kupelekea vifo hivyo vya watu 8.

                            Na, Lumemo blog

Post a Comment

 
Top