GuidePedia

0

Mbunge wa jimbo la songwe Philipo Mulugo iliyesimama akiongea na washiriki wa mafunzo hayo.


Mbunge wa viti maalumu Dr, Mery Mwanjelwa na Mbunge wa jimbo la songwe Philipo Mulugo wakicheza wimbo uliyoimbwa na washiriki wa semina katika ukumbi OTTU.

Mery Mwanjelwa na Philipo Mulugo wakibadilishana mawazo mara baada ya kuingia katika ukumbi huo



Washiriki wa mafunzo wakimsikiliza mgeni rasmi katika ukumbi huo mara baada ya wasili.

Moja kati ya washiriki wa mafunzo Bi, Mery Malema akisoma risala waliyoiandaa kwa mgeni rasmi

Mkufunzi wa mafunzo hayo Bw, Israel Ilundu akiwaelekeza jambo washiriki kabla ya kuwasili mgeni rasmi.




Mgeni rasmi Philipo Mulugo akikabidhi zawadi zilizoandaliwa na washiriki kama shukrani kwa baadhi ya viongozi akiwemo mkufunzi na Mery Mwanjelwa.


Hii ni meza iliyoandaliwa kwaajili ya vyakula mara baada ya kumaliza kufunga mafunzo hayo.





Viongozi wanawake wa nyanja mbali mbali katika chama cha Mapinduzi CCM mkoani mbeya wamepatiwa mafunzo yanayohusu mbinu za kukabiliana na changamoto za uongozi pindi wawapo marakani.

Mafunzo hayo yaliyoendeshwa kwa muda wa siku tatu katika ukumbi wa OTTU kabwe jijini mbeya yaliandaliwa na mbunge wa viti maalumu mkoa wa mbeya Dr. Mery Mwanjelwa ambapo jana ndiyo kilele chake.

Katika kufunga mafunzo hayo mgeni rasmi aliyealikwa kwaajili ya kufunga ni Mbunge wa jimbo la songwe Mh, Philipo Mulugo ambapo katika kujibu risala iliyoandaliwa na washiriki wa mafunzo hayo aliwataka washiriki kutumia vyema elimu waliyoipata na kuacha kurubuniwa na baadhi ya wanasiasa wenzao wasio aminifu.

Aidha Mulugo amesema kumekuwa na tabia kwa baadhi ya wanachama wa chama cha CCM kukubali kununuliwa na viongozi ambao siyo waadilifu, hivyo kupitia madfunzo hayo anaamini kuwa kutakuwa na mabadiliko makubwa kufuatia uchaguzi mkuu ujao.

Mulugo alimpongeza Mbenge wa viti maalumu Mh, Mery Mwanjelwa kwakuwaandilia wanawake hao mafunzo hayo kwani endapo watayafanyia kazi ipasavyo yataleta tija kwao na jamii kwa ujula.

Awali washiriki wa mafunzo katika risala yao waliyoiandaa walimshukuru Mbunge Mwanjelwa kwakuwaandalia mafunzo na kuahidi kupitia mafunzo hayo hawatarubuniwa na viongozi wasio adilifu na kumtaka mbunge Mwanjelwa kuendelea na moyo huo wa kujitolea kwani mafunzo kama hayo mara nyingi yamekuwa yakitolewa kwa malipo lakini kwakupitia Mbunge huyo wameyapata bure.

Kwaupande wake Mbunge wa viti maalumu Mh, Dr Mery Mwanujelwa amesema amefurahishwa sana na washiriki hao namna walivyoweza kupokea kwa haraka kitu ambacho walichokuwa wanafundishwa pamoja na wakufunzi waliyokuwa wakiwafundisha washiriki hao kutoka katika shirika la FACE la Ujerman linalojihusisha na mafunzo ya utawala bora kwa viongozi.

                    Na, Lumemo blog







Post a Comment

 
Top