GuidePedia

0

Mratibu wa mafunzo hayo kutoka TGNP Alphonce Stima akifanya maandalizi ya mafunzo.

Afisa mtendaji wa kijiji cha Ilota kata ya mshewe Maclaud Mwasanjingu akisoma mrejesho wa mafunzo ya siku ya kwanza.

Muwezeshaji wa  mafunzo Lawrence Chuma akifanya maandalizi ya mafunzo.

Washiriki wa mafunzo wakiwa darasani wakimsikiliza muwezeshaji wakati mafunzo yakiendelea ukumbini.



Washiriki wakiwa katika foleni ya chakula cha mchana baada ya mafunzo.

Washiriki wakiwa katika picha ya Pamoja mara baada ya kufunga mafunzo 

 

WATUMISHI wa Halmashauri, ya Wilaya ya Mbeya vijijini,watendaji na wanahabari wametoa wito kwa serikali kupanga bajeti halisia iliyoibuliwa na wananchi  itakayokidhi mahitaji na usimamizi mzuri wa rasilimali   ili iweze kunufaisha jamii ya watanzania walio wengi badala ya kunufaisha wachache.
 

Wito  huo umetolewa na  washiriki wa mafunzo ya utawala bora na bajeti, yaliyoandaliwa na mtandao wa jinsia Tanzania Gender Networking Programme (TGNP) yaliyofanyika katika ukumbi wa Coffee Gardan uliyopo eneo la Sokoine jijini Mbeya, ambapo wamesema kuwa endapo serikali itazingatia matakwa ya miradi iliyoibuliwa na wananchi malalamiko hayatakuwepo na imani kwa serikali itaongezeka.

Baadhi ya watumishi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya vijijini  wakizungumza na Blog hii kwa nyakati  tofauti  wametoa maoni yao  kwamba nivema serikali ikapanga bajeti inayolingana na mapato yaliyopo

Afisa mtendaji wa Kijiji cha Njelenje   Kata ya Mshewe  Emanuael Kalimoja ameshauri  jamii ianze kujenga utamaduni wa kupanga bajeti kuanzia ngazi ya  familia  huku Afisa elimu shule za msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya Wende Mbilinyi amesema tatizo kubwa viongozi wa serikali wanapanga bajeti bila kuweka vipaumbele vya kuangalia matumizi na mapato yanayopatikana.

Kwa upande wake  mshauri elekezi wa mafunzo hayo, Lawrence Chuma akizungumza mara baada ya kuhitimisha mafunzo hayo kwa awamu ya kwanza amesema changamoto zilizopo katika kufikia dhana ya utawala bora ni kutokana na baadhi ya viongozi kutokubali wananchi wanapotaka kuhoji maswali ili kujua mustabali wa miradi ya maendeleo yao.

                          

                              Na, Lumemo blog




Post a Comment

 
Top