GuidePedia

0


Muwezeshaji wa mafunzo ya ufuatiliaji wa rasilimali za umma Lawrence Chuma













Inaelezwa kuwa chanzo cha baadhi ya viongozi wa umma kutokuwa na uhusiano mzuri na wanachi wao vijijini na kujiona ni miungu watu na   kuzikalia taarifa  za mapato na matumizi ni ukosefu wa ‘utawala bora’ na kutopevuka kwa demokrasia miongoni mwao.

Mtandao wa jinsia  Tanzania Gender Networking Programme (TGNP)  umetoa mafunzo katika ukumbi wa Coffee Garden Jijini Mbeya, kwa  baadhi ya  wananchi kupitia vituo vya taarifa na maarifa  kutoka Kata za Tembela,Mshewe na Ijombe wakiwemo na wanahabari ili kuwajengea uwezo na ufahamu wa haki zao katika ufuatiliaji  hali inayowasabaisha  kupaza  sauti zao   kwa watendaji kuacha kuwachukulia kama wapinga maendeleo pindi wanapofuatilia taarifa za  miradi  yao.

Sarah Jailos ni ni mmoja kati ya washiriki wa mafunzo hayo ambeye pia ni Mwenyekiti wa kituo cha taarifa na maarifa cha Twigushe ,Kata ya Ijombe mkoani Mbeya kumekuwa na changamoto kati yao na viongozi wao pindi wanapotaka kupata taarifa ya miradi yao, viongo hao wamekuwa wakiwaita ni wapinga maendeleo.

Aidha, Sabina Mwalyego ambaye ni  Mwenyekiti wa kituo cha taarifa na maarifa Kata ya Mshewe amesema changamoto kubwa alioipata ni baada ya Serikali kuwapatia fedha zaidi ya sh,mil. 31 kwaajili ya kujenga nyumba tatu za walimu ambapo mkuu wa shule hiyo alijenga nyumba moja yenye thamani ya sh, mli.5  badala ya nyumba tatu kama ilivyokusudiwa ndipo wao kama viongozi wa kituo cha taarifa na maarifa walilazimika kufuatilia kwa ukaribu ili kubaini ubadhirifu aliyoufanya mkuu huyo.

TGNP ilianza  kutoa mafunzo  ya  dhana ya utawala  bora  na suala la bajeti kwa watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Mbeya vijijini,madiwani,wanahabari na watendaji wa kata na vijiji  na hatimaye kwa wananchi kupitia  vituo vya taarifa na maarifa ambavyo vinafanya kazi na mtandao huo wa kijamii tangu september 16 mwaka huu, lengo likiwa   kushirikishana  na kujifunza  umuhimu wa kufuatilia matumizi na rasilimali za umma  ili kuboresha  uwajibikaji,utawala bora katika ngazi hizo.

Mwisho.

                              Na, Lumemo blog

Post a Comment

 
Top