GuidePedia

0


WANANCHI wilayani Rungwe mkoani Mbeya wameihoji ahadi ya ujenzi wa barabara toka Ruangwa masoko,mwakaleli hadi katumba yenye kilometa 48 kwa kiwango cha rami iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete mwaka 2005 wakati akiomba kura kwa wamanchi wa jimbo la Rungwe magharibi.

Akizungumza na waandishi wa habari  walipotembelea barabara hiyo kwa niaba ya wananchi wengine Staford Mwaikape mkazi wa kata ya Bulyaga alisema Rais Kikwete  alipokuwa akiomba kura alitoa ahadi hiyo kuwa atatengeneza barabara huyo kwa muda wa miaka mitatu lakini hadi anamaliza muda wake hakuna kinachoendelea.

Alisema kuwa awali waliwahi kwenda kwa mbunge wao Prof. David Mwakyusa kumshinikiza amkumbushe Kikwete kuitengeneza barabara hiyo lakini  walikwama baada ya mbunge wao kuhamia Dar,es,salaam huku akija kwa mwaka mara moja na wao kukosa sehemu ya kupeleka malalamiko yao.

Aliongeza kuwa kutotekelezeka kwa miradi ya maendeleo kwa nchi hii inatokana na baadhi ya viongozi kutosimamia misingi ya utawala bora na kwamba wao kama wananchi wamepata somo kutokana na viongozi kutowajibika katika shughuri za kijamii  kama ilivyo kwa Rasi Kikwete.

“Aiingii akilini Rais kutoa ahadio alafu ashindwe kuitekeleza huku mbunge nae ashindwe kumkumbusha na ndiyo maana viongozi wengi wamekuwa wababaishaji kutokana na viongozi wao wakuu kutothamini misingi ya utawala bora”alisema Mwaikape.

Mbunge wa jimbo la Rungwe Magharibi (CCM) Prof,David Mwakyusa alipotakiwa kulizungumzia sakata hilo la kutosimamia masuala ya kimaendeleo na kutomkumbusha Rais kutimiza ahadi hiyo huku akiishi Dar,es,salaam na kuja kwa mwaka mara moja jimboni mwake kwa njia ya mtandao hakuweza kujibu.

Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) wilayani humo Ally Mwakalendile mbali na kukiri kuwepo na ahadi hiyo ya Kikwete alisema upembuzi yakinifu umekwisha fanyika kwa kuanzia ujenzi wa kilometa 1.5 upande wa Rungwe magharibi na upande wa mashariki kilometa 10.

“ni kweli Rais Kikwete aliahidi kuijenga barabara hiyo na kwa kuwa ujenzi umechelewa wananchi wanahaki ya kuidai lakii hata kama Kikwete akimaliza muda wake Rais ajae ataikamirisha hivyo wananchi wasiwe na hofu juu ya ujenza wa barabara hiyo”alisema Mwakalendile.

Mkuu wa wilaya hiyo Chrispin Meela kwa upande wake alisema kuwa wananchi wana haki ya kuidai barabara hiyo kwa kuwa Rais aliahidi na kuwa kwa kuwa imechelewa wananchi wasiwe na hofu kwa kuwa tayari taratibu za awal za ujenzi zimekwisha anza.

Kuhusu miradi mingine kujengwa chini ya kiwango na mengine kuchakachuliwa Meela alisema tayari Serikali kupitia chama cha mapinduzi imekwisha chukua hatu na tayari waliosababisha uchakachuaji huo wameanza kuhojiwa.

                        Na, Lumemo blog

Post a Comment

 
Top