GuidePedia

0

Mwezeshaji Bi, Groria Mafule akiendele kutoa mafunzo katika ukumbi huo.

Mwezeshaji Bi, DorothyMbilinyi pia akitoa mafunzo kwa washiriki katika ukumbi huo.

Mratibu wa mafunzo hao kwa mkoa wa mbeya Alphonce Stima  akiwa katika ukumbi wa mafunzo.

 

Washiriki wa mafunzo wakiwa darasani wakiwasikiliza wawezeshaji wakiwafundisha.




Mtandao wa jinsia, Tanzania Gender Networking Programme (TGNP) unaendelea kutoa mafunzo kwa viongozi wa nyanja mbali mbali katika ukumbi wa Malisho uliopo Uyole jijini mbeya yenye lengo la  kuona umuhimu wa kushiriki chaguzi za serikali za mitaa na uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka 2015.

Akizungumza na mtandao huu nje ya ukumbi huo mratibu wa mafunzo hayo Alphonce Sitima amesema malengo ya mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo viongozi hao kuona umuhimu wa kushiriki kikamilifu katika chaguzi mbali mbali za serikali.

Aidha Sitima amesema mafunzo hayo yamewalenga wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kwani makundi hayo yamekuwa mstari wa nyuma kutokana na hali zao zilivyo na kujikuta wakipuuzwa pindi wanapotaka kutoa maoni yao.

Stima ameongeza kuwa Mtandao huo umekuwa ukifanya kazi na kituo cha haki za binadaumu kwa muda mrefu sasa kwa lengo la kuondoa dhana ya unyanyasaji wa kijinsia ili waweze kujiamini na pindi inapotokea nasafi ya uongozi waweze kuingia katika kinyang’anyoro hicho.

Kwa upande wao washiriki wa mafunzo hayo wamesema kupitia mafunzo hayo wamepata uwezo wa kimaamuzi katika uchaguzi wa serikali za mitaa hata katika uchaguzi mkuu wanaotarajia kufanyika mwakani.

“Sisi kama washiriki wa mfunzo hayo kwanza tumenufaika kwa kiasi kikubwa sana na tumepata uwezo wa kuwa na maamuzi katika jamii inayotuzunguka tofauti na siku za awali maana siku za nyuma ilikuwa tofauti kidogo katika uelewa wetu ukilinganisha na sasa baada ya kupata mafunzo haya” walisema washiriki hao.

Bahati Bukubilu ni mmoja kati ya washiriki katika kundi la walemavu aliyetokea mbalizi jijini  amesema kwa upande wake amefurahishwa sana na mafunzo hayokwani hakuwai kushiriki katika mafunzo kama hayo. 

“mimi binafsi nimefurahi sana kupitia mafunzo haya maana hii ndo mara yangu ya kwanza kupata mafunzo kama haya hivyo nimetambua umuhimu wa kushiriki katika chaguzi mbali mbali zinazotarajia kufanyika hapa ncini pia naiomba serikali kututengenezea miundombinu katika sehemu mbali mbali hasa ofisi za serikali na mashirika binafsi ili tuweze kuingia kwa urahisi maana serikali imekuwa ikituhaidi kuhu kutengeneza miundombinu masipo kukamilisha” Alisema Bahati.
 
Hata hivyo mafunzo hayo yanatarajia kuendeshwa kwa muda wa siku tatu ambapo leo ni siku ya pili tangu kuanza kwake na yanarajia kuisha september 24 mwaka huu.


                          Na, Lumemo blog




Post a Comment

 
Top