GuidePedia

0
SHIRIKA la The Struggle For Community Support Alliance (SCSA) yenye makao makuu yake wilayani Kyela mkoani Mbeya jana limetangaza neema kwa wananchi wa wilaya hiyo ya kuwaletea mradi wa gesi asilia au gesi hai (BIOGAS) utakao anza mwezi march mwaka huu.

Akizungumza jana na waandishi wa habari ofisini kwake mwenyekiti wa shirika hilo kitaifa Dk,Abraham Mwanyamaki alisema asasi yake imesajiliwa kwa ngazi ya Taifa kwa ajili ya kufanya kazi za kusaidia jamii upande wa Afya,Elimu,Michezo,Mazingira na ujasilia mali na kuwa kwa mwaka wa kwamza tayari wamesaidia Sekta ya elimu na michezo.

Alisema kuwa mwaka huu wa 2014 Shirika lake litajikita kuleta mradi wa Gesi hai kwa kila kata ambapo wananchi watatakiwa kujiunga katika vikundi kwa ajili ya kuwezeshwa kupatiwa mradi huo ambao utawapunguzi tatizo la kutembea umbali mrefu kufuata kuni na mkaa kwa ajili ya kupikia na badara yake watatumia gesi hai itakayotengenezwa na wao wenyewe.

Mwanyamaki aliongeza kuwa Shirika lake kwa kushirikiana na wafadhiri mbalimbali wakawemo wakala wa umeme vijijini (REA) ambao wamewapatia mitambo yakuanzia kufunga kwenye kila kata ili wananchi waanze kunufaika na mradi huo ambao utasaidia kupunguza uchafuzi wa mazingira kwa kuwa taka ngumu ndizo zitakazotumika katika mradi huo.

Alisema kuwa anawataka wananchi kuwa tayari kuupokea kwa mikono miwili mradi huo ambao wataanza kufunga mitambo miwili kwenye kata za Ipande na Kasumulu kwa kufuata maelekezo kutoka kwenye Halmashauri ya Wilaya Idara ya mifugo ambao ni wadau wakubwa wa mrad huo.

Aliongeza kuwa mwezi wa tatu mwaka huu watakapofunga mitambo hiyo kwenye kaya hizo watatoa mafunzo kwa wananchi watakao jiunga kwenye vikundi namna ya kutumia mradi huo ili kuleta ufanisi katika matumizi sahihi ili wasipate madhara.

Hata hivyo Mwenyekiti huyo amewasisitiza wananchi hao kuacha kusikiliza propaganda zinazoenezwa na baadhi ya wanasiasa wasioitakia mema wilaya hii na kuwa katika suala la maendeleo siasa ikae pembeni kwani inakwamisha juhudi za kumkwamua mwananchi katika lindi la umasikini.

Post a Comment

 
Top