GuidePedia

0
WANANCHI wa kijiji cha Lema kata ya Busale wilayani Kyela mkoani Mbeya wameilalamikia Idara ya elimu iliyochini ya Halmashauri ya wilaya hiyo kwakutosikiliza kilio chao cha kuwaletea waalimu katika shule yao ya  msingi Lema.
 
Wakizungumza na waandishi wa habari jana kwa nyakati tofauti kijijini humo wananchi hao walidai kuwa kwa muda mrefu shule hiyo imekuwa haina waalimu huku idadi ya wanafunzi ikizidi kuongezeka lakini Idara hiyo imeshindwa kupeleka waalimu katika shule hiyo.
 
Walisema shule hiyo inawaalimu wanne kati yao wavulana wapo wawili na wanaume wawili huku wanafuzi wakifikia mia sita kitu ambacho ni kinyume na utaratibu wa wizara huku wanafunzi wa shule hiyo wakikosa haki yao ya msingi katika kupata elimu stahiki.
 
mwandishi wa habari hizi alifika katika shule hiyo na kujionea uhalisia wa kero hiyo ulioenda sambamba na kuongea na viongozi wa kijiji hicho ambao ni mwenyekiti wa kijiji Christopha  Lukali na Mratibu wa elimu wa kata Umbege Lugano ambao walikiri kuwepo na kero hiyo na kuwa tayari wamelipeleka suala hilo kwenye idara usika.
 
Diwani wa Kata hiyo Ezekia Msyani alisema kuwa ni kweli shule hiyo inawaalimu wanne huku wanafunzi wakiwa 600 na kwamba walikwisha fanya mkutano mkuu wa kijiji kulizungumzia suala hilo kuhusu uhitaji wa waalimu na muhtasari wa mkutano huo waliupeleka kwenye ofisi ya elimu na hivi sasa wanasubiri utekelezaji wa ombi lao.
 
Aliongeza kuwa shule hiyo imekamilika kila idara na haina tatizo lolote isipokuwa upungufu wa waalimu kitu ambacho kinadidimiza elimu kwa wanafunzi wanaosoma kwenye shule hiyo na kwamba aliiomba idara hiyo kuliangalia suala hilo kwa jicho la tatu ili kunusuru hali hiyo itakayo didimiza elimu kwa wanafunzi wanaosoma kwenye shule hiyo.
 
Afisa elimu msingi wa wilaya hiyo Claud Bulle alipozungumza na gazeti hili ofisini kwake alikiri kuwepo na upungufu huo na kudai kuwa hilo ni tatizo kubwa ikichukulia waalimu wanne kwa wanafunzi mia sita ni hatari kubwa inayoweza kushusha ufauru kwa wanafunzi wa shule hiyo.
 
Aliongeza kuwa kwa kuliona hilo idara yake ilipeleka maombi ya uhitaji wa waalimu kwa wilaya nzima na watatoa kipaumbele cha kupeleka waalimu wengi katika shule hiyo na kwamba katika sheria za wizara ni kuwa wanafunzi alobaini wanatakiwa wafundishwe na mwalimu mmoja kwa wanafunzi mia sita waalimu wanne ni pengo kubwa la waalimu lilipo katika shule hiyo.
 
Aliwataka wananchi wa kijiji hicho kuwa wavumilivu kwani wao kama idara wanalifanyia kazi tatizo hilo na kuwa watapeleka waalimu wa kutosha katika shule hiyo pindi watakapoletewa waalimu wapya mwaka huu.
 
 
                                                                       (Habari na Ibrahim Yassin)

Post a Comment

 
Top