GuidePedia

0



Hili ndiyo eneo la lililofyekwa miti  na hii ndo miti iliyofyekwa na hawa ni baadhi ya wananchi wamaeneo hayo.
..............................................................................................................................................................


Wanachi wa kijiji cha Itamboleo kata ya Itamboleo wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya wameulamikia uongozi wa Kata na Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya kwa kutochukua hatua baada ya umoja kikundi cha wafugaji wa Matebete kuuza ardhi ya kijiji kwa watu binafsi.

Mwenyekiti wa kijiji Samwel Kaganga amesema kuwa eneo hilo lilitolewa na serikali kwa ajili ya lanchi ya mifugo lakini badala ya kutumia eneo hilo kama ilivyokusudiwa na serikali kikundi hicho kimefyeka baadhi ya maeneo na mengine kuyauza kinyume cha sheria.

Taarifa zimetolewa ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri lakini hakuna utekelezaji wowote ambao umefanyika na kuwafanya wananchi waliokuwa wanamiliki mashamba hayo kuwa vibarua ili waweze kujikimu na njaa.
Mwenyekiti Kaganga ameiomba serikali kulipatia ufumbuzi suala hili ili kuepusha uharibifu mkubwa wa mazingira unaofanywa na wafugaji kwa kukata miti hovyo ili kupata mashamba ambayo huyauza kwa wafanyabiashara wakubwa wa Chimala na Mbeya.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Mbarali Gulamhusein Kiffu ameahidi kulifuatilia suala hilo ili kuepusha vurugu na pia kuzuia uharibifu wa mazingira ili kuepusha Mbarali kugeuka jangwa.

Post a Comment

 
Top